• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za ofisi |
Buhigwe District Council
Buhigwe District Council

Jamuhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Msingi Mkuu
    • Mpango Mkakati
  • Utawala
    • Muundo Wa Utawala
    • Idara
      • Utawala Na Utumishi
      • Mipango, Takwimu Na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha Na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Secondari
      • Maji
      • Mifugo Na Uvuvi
      • Ardhi Na Maliasili
      • Maendeleo Ya Jamii Na Ustawi Wa Jamii
      • Ujenzi Na Zimamoto
      • Kilimo,Umwagiliaji Na Ushirika
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi Wa Ndani
      • Habari Na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kiutalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
      • Kuonana na Mhe.Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Inayotarajiwa Kufanywa
    • Miradi Inayoendelea Kufanywa
    • New Planned Project
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Other Fomu
    • MpangoKazi
    • Baraza-Madiwani
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Kikao maalumu cha Baraza la Biashara wilaya Buhigwe

Posted on: October 3rd, 2017

Tarehe 29.09.2017 Wanakamati wa Baraza la Biashara la Wilaya ya Buhigwe kwa kushirikiana na Wajumbe wa Baraza la Biashara la Wilaya sanjari na Baraza la Waheshimiwa Madiwani walikutana katika ukumbi wa CHAMPANDA wilayani humo kujadili na kupitisha ajenda kuhusu kupanua fursa za biashara na uwekezaji katika Wilaya ya BuhigweMwenyekiti wa KAMATI TENDAJI Baraza la Biashara Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe Ndugu Anosta Nyamoga alifungua Kikao mnamo saa 11:45 asubuhi kwa kuanza na utambulisho wa meza kuu, ambapo aliongoza utambulisho huo kwa kuanza na yeye mwenyewe, kisha mwenyekiti TCCIA (Bw. Azaria Asheri), Meneja LIC-Kigoma (Dr. Betty Mlingi), mwakilishi TNBC ( Bw. Annosisye Mwamsiku), Katibu Tawala Wilaya ya Buhigwe (Ndg. Peter Masindi) pamoja na wajumbe wa kamati tendaji.

Meneja (LIC- Kigoma) alielezea umuhimu wa kujumuisha Baraza la Madiwani na wajumbe wa Baraza la Biashara ili kwamba wajadili kwa pamoja kutatua changamoto zinazokabili ukuaji wa uchumi ndani ya Wilaya. Meneja LIC- Kigoma aliongeza kwamba majadiliano baina ya Baraza la Biashara na Baraza la Madiwani yatafanya mabaraza yawe na nguvu hata mradi wa LIC ukimalizika na Baraza la Biashara liweze kujiendesha lenyewe. Waheshimiwa madiwani watapata fursa ya kujua kinachoendelea kwenye maeneo yao ikiwa ni pamoja na changamoto za kiuchumi zilizopo kwenye kata zao na utatuzi wake.

Kituo cha Biashara (One Stop Business Centre) kilichukuliwa kama mfano ambapo kilionekana kuwa kigeni kwa baadhi ya waeshimiwa madiwani kutokana na kutojua kinachojadiliwa kwenye vikao vya Baraza la Biashara Wilaya na maazimio yake. Hivyo kuletwa pamoja kwa mabaraza hayo mawili ilionekana ni muhimu ili kupisha sintofahamu zinazoweza kuibuka kutokana na kwamba Waheshimiwa Madiwani wachache ndio wanaofahamu uwepo wa Baraza la Biashara la Wilaya.


Agenda zilizo jadiliwa nikama zifuatazo:-

AJENDA 1: UFAFANUZI WA BARAZA LA BIASHARA, MUUNDO WAKE NA MAJUKUMU YA WAJUMBE NA UFAFANUZI JUU YA MRADI WA LIC.

Ajenda hii imegawanyika katika makundi makuu mawili nayo ni yafuatayo:-

  • UFAFANUZI WA BARAZA LA BIASHARA, MUUNDO WAKE NA MAJUKUMU YA WAJUMBE.

 

 

                             BARAZA LA BIASHARA TAIFA (TNBC)

Ni Sekretarieti / Chombo kilicho undwa kwa waraka wa Rais Na.1 wa mwaka 2001 na kutangazwa kwenye Gazeti la Serikali Na. 691 - 28 Sept 2001. Kwa lengo la kuboresha mazingira ya Biashara kwa maendeleo ya Taifa.

                                                   

  • MUUNDO WA BARAZA LA BIASHARA LA WILAYA

Kaburasha la ajenda hii limeambatanishwa kwa lengo la kuwapa wajumbe fursa ya kupitia wakati mratibu akifafanua ajenda hii

AJENDA 2: ONE STOP BUSINESS CENTRE.

Meneja mradi wa LIC mkoa wa Kigoma(Dr. Betty Mlingi) alieleleza juu ya kujengwa kwa kituo cha huduma za Biashara cha Wilaya (One Stop Business Centre) na Ufafanuzi juu ya mradi wa LIC.


AJENNDA 3: MAFANIKIO YA BARAZA LA BIASHARA WILAYA YA BUHIGWE

  • Agenda hii ilifafanuliwa na Afisa Biashara Wilaya ya Buhigwe (Bw. Onesphory John)

A: UTANGULIZI.

Baraza la Biashara la Wilaya ya Buhigwe liliundwa Tarehe 19.05.2016 na Mwenyekiti wa Baraza na Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe wa wakati huo Mhe. Marry Tesha Onesmo. Mwenyekiti wa Baraza hilo aliongea mambo mengi kuhusu umhimu wa mabaraza ya biashara kwa sekta ya Umma na Binafsi katika kutatua changamoto za kibiashara zinazokwamisha ukuaji wa Uchumi katika maeneo husika. Mheshimiwa Mwenyekiti wa Baraza alienda mbali zaidi na kusema mazungumzo ya kirafiki baina ya sekta hizi mbili ndio yanaweza kutatua changamoto mbalimbali za biashara na kuchumi, na kushauri kwamba kuwe na umoja baina ya sekita hizi juu ya utatuzi wa maswala mbalimbali.

B: MAFANIKIO.

Uwepo wa jukwaa la majadiliano kati ya sekta ya umma na sekta binafsi.

Uanzishwaji wa baraza la biashara ndani ya Wilaya imeongeza fursa ya majadiliano baina ya sekta ya umma na sekta binafsi. Kabla ya baraza la biashara kuanzishwa sekta binafsi ilikuwa inapata wakati mgumu hasa linapokuja suala la kujadili mambo yanayokwamisha ukuaji wa biashara na upatikanaji wa fursa za uwekezaji Wilayani. Baraza hili limekuwa likiwakutanisha wadau na taasisi za kifedha kama vile NMB kwa lengo la kupata elimu juu ya masuala ya kifedha.

Wajumbe wa baraza la biashara wamejengewa uwezo wa kujenga na kutetea hoja. Kupitia mijadala na mafunzo yanayoendeshwa ndani ya baraza la biashara wajumbe wa sekta ya umma na sekta binafsi wameongeza ufanisi wa kuwasilisha na kutetea ajenda. Ajenda hizo zaweza kuwa ni changamoto zinazokwamisha ukuaji wa uchumi ndani ya wilaya ama ajenda zinazoibua fursa za uwekezaji na uboreshaji wa mazingira ya biashara.

 Baraza la biashara limeongeza wigo wa upatikanaji wa elimu juu ya masula ya biashara, elimu ya mlipa kodi, ujasiriamali na uwekezaji.

Ndani ya baraza la biashara elimu ya biashara, mlipa kodi, ujasiriamali na uwekezaji hutolewa. Elimu mojawapo ni kuhusu uhararishaji wa biashara pamoja na mfanyabiashara kuwa na leseni ya biashara, misingi ya uanzishwaji wa biashara ni mambo gani mfanyabiashara inabidi kuzingatia. Baraza limesaidia wafanyabiashara kupata elimu juu ya ulipaji kodi.

Baraza la biashara limesaidia kubaini matatizo yanayoikabili sekta binafsi.

Mijadala inayoendeshwa ndani ya vikao vya baraza la biashara imewezesha kubaini ni matatizo gani ama ni changamoto zipi sekta binafsi inakumbana nazo katika utekelezaji wa shughuli za kiuchumi. Mojawapo ya matatizo hayo ni kama yalivyoainishwa hapa chini:-

  • Kutokuwa na masoko ya uhakika ya bidhaa na mazao yazalishwayo na wafanyabiashara na wananchi kwa ujumla.
  •  Migogoro kama uvunjwaji wa vibanda eneo la mnanila zoezi lililotekelezwa na TANROAD.
  • Kukosekana kwa huduma za kifedha ndani ya walaya.
  • Uwepo wa vizuizi vingi barabarani, changamoto hii imepelekea kuongezeka kwa gharama za kuendesha biashara.

AJENDA 4: KUBORESHA MAZINGIRA YA BIASHARA

  • UJENZI WA SOKO LA MUNANILA NA STENDI YA KUEGESHEA MAGARI.

Soko la Munanila lilivunjwa mwaka 2004 baada ya serikali kuwa na mpango wa kupitisha barabara ya lami katika eneo la soko la kutoka Kigoma hadi Munanila. Mpango huu wa serikali ulikuwa kuondoa kero au tatizo la usafirishajiwa bidhaa,mazao na abiria kutoka Manyovu hadi Kigoma.

Baada ya kuvunja vibanda vya kudumu 120 vilivyokuwa vimejengwa katika eneo hilo tangu mwaka 2004, hadi sasa hakuna mpango uliowazi wa serikali kufidia vibanda hivyo na kutenga eneo lingine kwa ajili ya ujenzi wa vibanda vya Biashara.

Kwa maana hiyo Halmashauri inaendelea kupoteza mapato ambayo ingepata kutokana na;

  • Vyumba vya Biashara
  • Ushuru wa mazao mbalimbali.
  • Ushuru wa egesho wa magari (stendi)
  • UJENZI WA BARABARA YA KASULU HADI MANYOVU NA MUNANILA HADI MWAYAYA.

KASULU HADI MANYOVU.           

Barabara hii ni muhimu kwa kusafirisha abiria ,bidhaa mbalimbali za biashara na mazao ya kilimo. Gharama za usafirishaji katika barabara hii ni kubwa , mfano nauli ya abiria kutoka Manyovu hasi Kasulu ni Tsh 7,000/= (elfu saba). Gharama za usafirishaji zimekuwa juu kwa sababu ifuatayo;

Barabara hii imejaa mawe kiasi ambacho ni hatarishi kwa wenye magari kwa kupasuka tyres na kupasua vioo vya gari.

MUNANILA HADI MWAYAYA.

Barabara hii ni muhimu kwa kusafirisha mazao ya kilimo kutoka Mwayaya,Muhinda na Nyaruboza hadi katika eneo la soko kuu la Munanila.

Barabara hii haipitiki kipindi cha masika ambapo wakulima wanashindwa kufikisha mazao yao soko kuu la Munanila. Vilevile wafanyabiashara wa maeneo hayo hushindwa kusafirisha bidhaa za madukani katika vijiji hivi katika kipindi hiki.

MAONI: Barabara hii itengenezwe kwa kiwango cha Changarawe ili iweze kupitika kwa muda wote. 

  • MPANGO MAALUMU WA KUBORESHA MNYORORO WA THAMANI.        
  • ZAO LA MAWESE:

Zao hili hulimwa katika vijiji vya Kinazi na Janda. Pamoja na hamasa ya kuzalishwa/kulimwa kwa zao hili katika vijiji hivi, bado kuna changamoto ambazo zinarudisha nyuma uzalishaji wake.

Mfano;

  • Kukosekana kwa Soko rasimi la Mawese (Mnunuaji/ Mfanyabiashara kupanga bei na sio mkulima).
  • Vifaa duni vya kuchakata zao hili.
  • ZAO LA TANGAWIZI:

Pamoja na hamasa ya kulima/kuzalisha zao hili katika vijiji vya Munzeze, Kishanga na Kigogwe kuna changamoto ambazo zinarudisha nyuma uzalishaji wa zao hili.

Mfano;

  • Kukosekana kwa soko la uhakika.
  • Wanunuzi hutumia madalali walioko kijijini kununua zao hili kwa bei ya chini.

MAONI: Halmashauri itafute namna ya kutatua kero hizi kwa ujumla ili wananchi waendelee kuhamasika kuzalisha mazao haya.

  • MPANGO WA MATUMIZI BORA YA ARDHI (WAKULIMA NA WAFUGAJI).
  • WAKULIMA:

Kundi hili lielimishwe mpango wa matumizi bora ya ardhi.

Mfano;

  • Matumizi bora ya pembejeo
  • Utunzaji wa vyanzo vya maji
  • Kuacha kukata miti ovyo wakati wa maandalizi wa mashamba mapya.
  • Kuacha kuchoma moto ovyo.
  • WAFUGAJI:

Kundi hili lielimishwe juu ya mpango wa matumizi bora ya ardhi.

Mfano;

  • Kutumia malisho kwa usahihi (avoid overgrazing)
  • Kupunguza mifugo kulingana na eneo la malisho (carrying capacity )

MAONI: Halmashauri Kwa kuwatumia wataalaamu waliopo ihakikishe makundi haya ya Wakulima na Wafugaji wanaelimishwa kwa kina kuhusu swala la matumizi bora ya ardhi.

 

  • ELIMU YA BIASHARA, VIWANGO NA KODI:
  • Kipengele hiki kiliwasilishwa na Afisa Biashara Wilaya ya Buhigwe (Ndg. Onesphory John) akishirikiana na (Bi. Clara Mwamba) kutoka Sekretarieti.

ELIMU YA BIASHARA:

Elimu ya biashara ni pana kwa kuzingatia upana huo, leo tutaangazia elimu juu ya leseni za biashara na kadri tutakapo kuwa tunakutana katika maeneo mbalimbali ya wafanyabiashara na wananchi kwa ujumla tutazidi kujulishana mambo mengi zaidi kuhusiana na elimu ya biashara.

SHERIA YA LESENI ZA BIASHARA NA MAREKEBISHO YAKE (Business Licensing Act No 25 of 1972, Amendment 1980, 2014 and 2015).

Hapa chini ni ufafanuzi wa mambo ya msingi kwa wafanyabiashara na wananchi wanaotarajia kuanzisha biashara mbalimbali ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

                          MASHARTI YA KUPATA LESENI YA BIASHARA:

Mtu yeyote raia wa Tanzania anayo haki ya kupatiwa leseni ya biashara ili mradi awe  ametimiza  umri  wa  miaka  kumi  na  nane  (18)  mwenye  akili  timamu  na ambaye hajawahi kupatikana na kosa la jinai (katika kipindi cha miezi 12 iliyopita) na awe na eneo la kufanyia biashara linalokubalika kisheria. Kwa mtu ambaye siyo raia wa Tanzania anapaswa kuwa na Hati ya kuishi nchini daraja `A`(Residence permit class A) na nyaraka nyingine za usajili wa kampuni yake ndio aweze kufanya biashara nchini. 

  • UTARATIBU WA KUPATA LESENI YA BIASHARA: 

Mwombaji anapaswa kujaza fomu ya maombi TFN 211 kikamilifu na kuambatanisha kivuli cha:-

(i)        Certificate of Incorporation iwapo ni kampuni na Certificate of Registration and Extract kama ni jina la biashara. 

(ii)  “Memorandum and Article of Association”ambayo inaonesha kipengele ambacho kampuni hiyo inakiombea leseni ya biashara.

(iii)  Passport ya Tanzania au Kitambulisho cha uraia au Kitambulisho cha mpiga  kura  au  Cheti  cha  kuzaliwa  au  Hati  ya  kiapo(affidavit) kuonyesha kuwa ni Mtanzania na Mgeni Hati ya kuishi nchini daraja la “A” (Residnece Permit Class “A”). 

(iv)  Hati ya  kiuwakili  (Powers  of  attorney)  Iwapo wenye  hisa  wote  wa Kampuni  wapo  nje  ya  nchi,itolewe  kwa  mtanzania  ambaye  anaishi hapa.

(v)  Ushahidi wa  maandishi  kuwa  ana  mahali  pa,  kufanyia  biashara  (Kwa mfano hati za nyumba, mkataba wa upangishaji, risiti za malipo ya kodi za majengo au ardhi. 

(vi)  Hati ya kujiandikisha kama mlipa kodi TRA (TIN). 

vii) cheti cha kumaliza (uhitimisho) wa kulipa kodi (Tax Clearence Certificate).

(viii)  Kwa  leseni  zinazodhibitiwa  na  Mamlaka  mbalimbali  ,Kwa  mfano (TFDA,  EWURA,ERB,TPRI,TCRA,CRB,TALA,CAL)  n.k  lazima  mwombaji kuwa na leseni husika kabla ya kuomba leseni ya biashara.

(ix)  Hati  za  utaalam(  Professional  certificates)  kwa  biashara  zote  za kitaalam  mfano  Ushauri wa  kitaalam(  Consultancy),udaktari,urubani  wa ndege,uhandisi nk.

NB: Ikumbukwe kwamba maombi mapya  yanapitia  ngazi  zote  za  mwanzo  kwa  ajili  ya  ukaguzi kabla  ya kupitishwa  au  kupatiwa  leseni,ambazo  ni  Afya,  Mipango  miji  na  Afisa  biashara (W) au eneo ambapo biashara husika inayoombewa leseni itafanyika. 

  • MAKOSA YA LESENI ZA BIASHARA:
  • Kuendesha biashara bila leseni. 
  • Kuendesha  biashara  eneo  tofauti  na  linaloonyeshwa  kwenye leseni. 
  • Kutumia  leseni  moja  kufanyia  biashara  zaidi  ya  moja  au  maeneo mawili au zaidi. 
  • Kushindwa  kuonyesha  leseni ya  biashara  inapotakiwa  kufanya hivyo na Afisa  aliyeidhinishwa na Serikali. 
  •  Kutokuweka  leseni  ya  biashara  mahali  ambapo  inaonekana  kwa urahisi. 
  • Kutoa  maelezo  ya  uongo  ili  kupata  leseni  au  kukwepa  kulipa ada/kodi inayostahili. 
  • Kumzuia Afisa wa Serikali aliyepewa mamlaka ya kukagua kufanya kazi yake.

 

  • ADHABU:

Mtu  yeyote anayetenda  majawapo  ya  makosa  hapo  juu  adhabu  yake  ni  faini isiyopungua  Tshs.  200,000 na isiyozidi Tshs.  1,000,000 au kifungo kisichozidi miaka miwili (2) au faini na kifungo kwa pamoja.

  • MASHARTI YA UTUMIAJI WA LESENI: 
  • Mwenye leseni hataweka masharti yeyote kwa mnunuzi. 
  • Mwenye leseni atatoa risiti kwa mauzo yote. 
  • Mwenye  leseni  atafuata  sheria  ya  leseni  ya  Biashara  No. 25  ya  1972  na marekebisho yake.
  • Mwenye leseni hatatowa huduma/bidhaa ambazo hazizingatii viwango vya ubora,uliowekwa na vyombo vinavyotumika kisheria. 
  • Mwenye leseni anaweza kunyaganywa leseni na mamlaka iliyotoa wakati wowote  ikiwa  itaonekana  aliipata  kwa  njia  ya  danganyifu  au  amekiuka msharti ya leseni. 

ANGALIZO: Leseni za biashara hulipiwa ada na kuhuishwa (renew) kila mwaka kwa mjibu wa sheria ya leseni no. 25 ya 1972 na marekebisho yake ya 2014). Mfanyabiashara   anatakiwa kuhuisha leseni yake ya biashara ndani ya siku 21 tangu ilipomalizika na penalty ya 25% itatozwa kwa wanaochelewa na itakuwa ikiongezeka kwa 2% kila mwezi. 

  • VIWANGO: 
  • GS1

GS1 Tanzania ni taasisi iliyoanzishwa na serikali kupitia wizara ya Viwanda na Biashara na uwekezaji ikishirikiana na taasisi ya sekta binafsi  (TPSF) ikiwa na jukumu la kutoa alama za mistari za misimbomilia (Barcode) na mfumo wa ufuatiliki (Tracebility) kwa bidhaa za Tanzania. Taasisi hii ilisajiliwa na Brella na ilianza kazi zake za utoaji wa alama za utambulisho wa bidhaa Msimbomilia (Barcode)nchini kuanzia  tarehe 23 august 2011. Namba ya utambulisho wa bidhaa za Tanzania ni 620. Hivyo Barcode zote za Tanzania zinaanzia na namba 620.

  • Barcode ni nini?

Barcode ni alama za mistari za utambulisho wa bidhaa ambao kila bidhaa inatakiwa kuwa na Barcode yake endapo inatofautiana na nyingine kwa ladha,harufu,ufungashaji,ujazo,umbile,uzito na  rangi. Hii inamaanisha kila bidhaa inapotofautiana kwa chochote inapaswa kuwa na Barcode yake.

  • FAIDA ZA BARCODE KWA TANZANIA.

Bidhaa za Tanzania kukubalika masoko ya nje na ndani ya nchi. Ili bidhaa za Tanzania zikubalike kwenye masoko yaliyo rasmi ni lazima iwe na alama za utambuzi (Barcode).

  • Kuongeza mauzo ya bidhaa zilizo tayari (finished goods).Kama elimu ya umuhimu ya matumizi ya Barcode inawafikia wazalishaji itawasaidia kuongeza ufungashaji wa bidhaa zilizotayari na kupelekwa sokoni badala ya kupeleka bidhaa ghafi au kuuza malighafi.
  • Kuongeza ajira kwa vijana.
  • Kama vijana wakielezwa FURSA zilizopo kwenye soko kuhusiana na ufungashaji wa bidhaa ni wazi sekta hii itaajili vijana wengi na kupunguza fikra zakuajiriwa au kukimbilia mjini.ili bidhaa iweze kuuza inahitaji vitu vitatukifungasho bora, lebo iliyo bora na alama za utambuzi (Barcode).
  • Kurasimisha wafanyabiashara wengi zaidi.

          Ili uweze kupata Barcode kutoka GS1 Tanzania unahitaji kuwa na;

  • Leseni ya Biashara
  • Hati ya usajili wa kampuni
  • Jina la biashara
  • Namba ya utambulisho wa mlipa kodi (TIN namba)

Kwa kufanya hivi GS1 inakuwa inawarasimisha kutoka ufanyaji biashra holela mpaka walio rasmi.

  • FAIDA ZA BARCODE KWA MJASIRIAMALI/ MFANYABIASHARA.
  • Kutanua wigo wa soko.
  • Ili bidhaa yako ikubalike kwenye masoko yaliyo rasmi ni lazima iwe na barcode, hivyo basi hiki ni kigezo cha kwanza.
  • Barcode inakuwezesha kitanua wigo wa biashara yako toka masoko holela kwenda masoko yaliyo rasmi ya ndani na nje ya nchi.
  • Kupata mrejesho wa bidhaa yako sokoni.
  • Baada ya kupeleka bidhaa masokoni rasmi (supermarket) ni haki yako kurudi baada ya miezi mitatu,sita au mwaka mmoja ilikupata mrejesho wa bidhaa yako, hii itakusaidia kuweza kujua bidhaa yako inafanyaje sokoni,hii pia itakusaidia kujipanga katika uzalishaji na usambazaji (masoko).
  • Usahihi wa bei.
  • Kwenye maduka yaliyo rasmi hakuna kuomba kupunguziwa bei uchambuzi wa takwimu kibiashara.
  • Ili uweze faidika na huduma hii ni lazima uwe mwanachama wa GS1 na pia uwe na vitu vifuatavyo;
  • Leseni ya Biashara
  • Cheti cha usajili cha Brella (Certificate of Registration)
  • Namba ya utambulisho ya mlipa kodi (TIN namba).
  • SHIRIKA LA VIWANGO TANZANIA (TBS):

Shirika la Viwango Tanzania (TBS) ni shirika la Umma chini ya wizara ya Viwanda na Biashara lililoundwa chini ya Sheria ya Bunge namba 1 ya mwaka 1975 na kurekebishwa chini ya sheria namba 1 ya mwaka 1977.

  • Majukumu ya shirika hili ni kama yafuatayo:-
  • Kuelimisha umma juu ya masuala yote yanayohusu uwekaji na usimamiaji wa viwango pamoja na udhibiti wa ubora wa bidhaa viwandani.
  • Kuboresha bidhaa zinazozalishwa nchini kwa ajili ya masoko ya ndani na nje.
  • Kuthibitisha usahihi wa vipimo vinavyotumika viwandani na katika sekta za huduma na biashara.

Mpaka sasa TBS imeshaweka viwango zaidi ya 1600 katika Nyanja za kilimo na chakula, ngozi, kemikali, nguo, uhandisi, mitambo, umhandisi umeme na kadhalika.

  • Shirika hili linakagua viwango vya bidhaa mbalimbali katika maeneo tofauti kama ifuatavyo:-
  • Ukaguzi bandalini.

TBS huchukua sampuli wakilishi kabla bidhaa hazijapakuliwa katika bandari na mipaka yetu ili kuthibitisha ubora wa bidhaa husika. Bidhaa bora t undo huingia nchini.

  • Ukaguzi wa bidhaa nje ya nchi.

Bidhaa zinazoingia nchini kutoka nje ya nchi hukaguliwa katika nchi zinakotoka kabla kusafirishwa kuja nchini.

  • Ukaguzi wa kushitukiza sokoni.
  • TBS hukagua bidhaa kwa kushitukiza sokoni bila kumpa taarifa muuzaji. Bidhaa zisizofaa huharibiwa na muuzaji huchukuliwa hatua mbalimbali zikiwemo faini na kushitakiwa mahakamani.
  • FAIDA ZA BIDHAA ZENYE UBORA:

                   KWA MTEJA/MLAJI:

  • Humthibitishia mlaji kuwa bidhaa husika inafaa kwa matumizi husika.
  • Humhakikishia mlaji usalama wake kiafya na katika matumizi.

                  KWA MZALISHAJI:

  • Humpa uwezo mkubwa zaidi wa kushindana sokoni.
  • Humpa wateja zaidi.
  • Humkinga mzalishaji dhidi ya ushindani na bidhaa duni zisizo na ubora.
  • MAMLAKA YA CHAKULA NA DAWA (TFDA)

Mamlaka ya chakula na dawa (TFDA) ni taasisi iliyo chini ya wizara ya Afya na ustawi wa jamii yenye jukumu la kudhibiti ubora na usalama wa vyakula,dawa ,vipodozi na vifaa tiba.

TFDA imeanzishwa chini ya sheria ya chakula,dawa na vipodozi ,sura 219 na ilianza kutekeleza majukumu yake rasmi tarehe 1 Julai, 2003.

Mamlaka hii imejizatiti katika utoaji huduma bora ili kukidhi mahitaji na matarajio ya wateja wake kwa kuhakikisha ubora,usalama na ufanisi wa vyakula,dawa, vipodozi na vifaa tiba.

  • Kazi za TFDA (upande wa Dawa na Vipodozi)
  • Kusajili na kutoa vibali vya majengo ya kutengeneza na kuuza dawa,vipodozi na vifaa vya tiba.
  • Kukagua maeneo ya kutengeneza na kuuza dawa,vipodozi na vifaa tiba.
  • Kusajili dawa,vipodozi na vifaa tiba kabla ya kuruhusiwa kuuzwa soko la Tanzania.
  • Kutoa vibali vya kuingiza na kusafirisha nje ya nchi dawa,vipodozi na vifaa tiba.
  • Kazi za TFDA (upande wa usalama wa chakula)
  • Kusajili vyakula vilivyofungashwa kabla ya kuruhusiwa kuuzwa katika soko la Tanzania.
  • Kufanya tathmini ya athari zinazoweza kujitokeza kutokana na vyakula.
  • Kukagua shehena za bidhaa za vyakula katika vituo vya forodha na maghala ya kuhifadhia bidhaa hizi.
  •  
  • Wadau wa TFDA
  • Watengenezaji, waingizaji nchini, wasafirishaji nje ya nchi, wasambazaji na wauzaji wa vyakula, dawa, na vipodozi na vifaa tiba.
  • Idara za serikali na sekta Binafsi.
  • Walaji, watumiaji wa bidhaa na wananchi kwa ujumla.

Hivyo wafanyabiashara wanaojihusisha na biashara za uuzaji wa vyakula, vipodozi, na maduka ya dawa ni vizuri wakajisajili katika mamlaka hii ili kuhakikisha na kuuza bidhaa bora bila matatizo yoyote. Hii itaepuka uuzwaji wa bidhaa zilizoisha muda wake. (Expire) na kusababisha matatizo kwa mlaji/mtumiaji. Kwa kufanya hivyo kwa pamoja tutapambana na bidhaa duni na badia ili kulinda afya zetu.

  • ELIMU YA KODI:

Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) ni taasisi ya serkali iliyo na jukumu la kukusanya kodi ya serkali. Kila mwananchi anawajibika kulipa kodi kwa serkali iwe moja kwa moja hasa wafanyabiashara (Direct Tax) ama kwa kununua bidhaa iliyokwisha kamilika kwa ajili ya matumizi (Indirect Tax).

Mfanyabiashara anatakiwa kusajiliwa na mamlaka ya mapato ili kulipa kodi na usajili ukikamilika anapewa namba ya utambulisho wa mlipa kodi (Tax Identification Number – TIN) baada ya zoezi hilo atafanyiwa tathimini kulingana na biashara yake. Mfanyabiashara akilishafanya malipo atapewa cheti cha kumaliza kulipa mapato (Tax Clearence Certificate).

Mwananchi ambaye sio mfanyabiashara analipa kodi kutokana na vitu anavyo nunua kwa ajili ya matumizi ya nyumbani, kila unaponunua bidhaa yoyote kuna kiasi cha kodi kinakuwa kiko kwenye bidhaa hiyo.

  • Mwananchi anatakiwa kulipa kodi kwa maendeleo ya taifa, fedha zinazopatikana kutokana na kodi huelekezwa kwenye miradi ya maendeleo na huduma za jamii kama shule, hospitali

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI - 04.07.2023 June 23, 2023
  • KILA KHERI DARASA LA SABA September 12, 2023
  • TANGAZO LA AJIRA - OKTOBA 2023 October 09, 2023
  • TANZIA February 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • DED BUHIGWE ATEMBELEA VITUO VYA UANDIKISHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA.

    May 05, 2025
  • MATOKEO 2024 WALIMU NA WANAFUNZI WAPONGEZWA.

    April 17, 2025
  • BABA ASKOFU EMMANUEL BWATA AITIKIA WITO WA MKURUGENZI BUHIGWE.

    April 14, 2025
  • SHEREHE YA KUWAAGA WATUMISHI NA KUWAKARIBISHA WATUMISHI BUHIGWE YAFANA.

    April 13, 2025
  • Angalia zote

Video

Hospitali ya Wilaya ya Buhigwe kuanza kutoa huduma za Afya
Video Zaidi

Kurasa Za Karibu

  • Kuhamisha Mwanafunzi
  • Tovuti ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • FFARS USER GUIDE
  • PlanRep Documentation
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • Kata Zetu
  • Wahe. Madiwani
  • BEMIS

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Bunge La Tanzania
  • Ikulu
  • Bodi Ya Manunuzi na Ugavi
  • Wizara ya Ardhi
  • Wizara ya Elimu, Sayansi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Mji Mpya wa Bwega-Ofisi za Mkurugenzi

    Postal Address: P.O.Box 443 Buhigwe

    Simu Ya Mezani: 0282988460

    Simu ya mkononi: (+255) 782 500 333

    Barua Pepe: ded@buhigwedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma
    • Mwanzo

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Buhigwe. Haki zote zimehifadhiwa