• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za ofisi |
Buhigwe District Council
Buhigwe District Council

Jamuhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Msingi Mkuu
    • Mpango Mkakati
  • Utawala
    • Muundo Wa Utawala
    • Idara
      • Utawala Na Utumishi
      • Mipango, Takwimu Na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha Na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Secondari
      • Maji
      • Mifugo Na Uvuvi
      • Ardhi Na Maliasili
      • Maendeleo Ya Jamii Na Ustawi Wa Jamii
      • Ujenzi Na Zimamoto
      • Kilimo,Umwagiliaji Na Ushirika
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi Wa Ndani
      • Habari Na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kiutalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
      • Kuonana na Mhe.Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Inayotarajiwa Kufanywa
    • Miradi Inayoendelea Kufanywa
    • New Planned Project
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Other Fomu
    • MpangoKazi
    • Baraza-Madiwani
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

TASAF yazindua Mpango wa kunusuru Kaya maskini kipindi cha Pili - Buhigwe

Posted on: May 25th, 2021

Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) umezindua Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini kipindi cha pili cha awamu ya tatu katika Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe leo Jumanne, 25 Mei, 2021 katika ukumbi wa kanisa la Anglikana Dayosis ya Western Tanganyika Buhigwe mnamo saa 4:00 subuhi.

Madhumuni ya Kipindi cha Pili ni kuongeza fursa za kujiongezea kipato na kuboresha huduma za kiuchumi na kijamii kwa kaya za walengwa na kulinda maslahi ya watoto wao.

Kipindi cha Pili kitafikia malengo yake kwa kutekeleza shughuli mbali mbali kupitia sehemu kuu tatu ambazo ni uhawilishaji fedha ambao utaongeza kipato cha kaya na kuwekeza katika afya na elimu ya watoto, kuinua uchumi wa kaya kwa kujenga uwezo kwa kaya katika utunzaji rasilimali na kutengeneza njia mbadala na endelevu za ajira na kushiriki katika kazi za jamii na kupata kipato cha ziada kwa matumizi ya kaya kama chakula na kugharamia mahitaji mengine ya msingi na wakati huo wakiboresha miundombinu katika jamii na kupata ujuzi na stadi za maisha.

Hayo yamesemwa na Afisa Miradi ya Jamii TASAF makao makuu (Ndg. Henry Mbago) kwa niaba ya Mkurugenzi wa TASAF Tanzania wakati akisoma risala kwa Mgeni rasmi Mhe. Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe Col. Michael M. Ngayalina


Afisa Miradi ya Jamii TASAF makao makuu (Ndg. Henry Mbago akisoma risala kwa Mgeni rasmi

Aidha Ndg. Mbago aliongeza kuwa walengwa wa Mpango huu ni Kaya zinazoishi katika hali duni katika vijiji vyetu ambapo wanufaika ndani ya kaya ni watoto chini ya umri wa miaka mitano(5) wanaoenda Kliniki, Mama mjamzito na watu wenye ulemavu.

Katika Hotuba yake, Mgeni rasmi Mhe. Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe ameagiza kwamba Pesa ya ruzuku ya TASAF kwa walengwa isiishie kula nyama choma na  kulewa pombe isipokuwa zitumike kuibua miradi itakayo imarisha uchumi wa kaya mfano, ujasriamali, kilimo, ufugaji n.k

Kwa upande wa Viongozi na wataalamu waliohudhuria kikao kazi hicho, amewasihi kuwa mabalozi wazuri wa TASAF kwa kukemea vitendo vya udanganyifu wakati wa kuandikisha kaya mpya, wakati wa kubaini kaya duni na kwamba kila wanapofanya ziara za kikazi wazungumzie umuhimu wa TASAF. 

Walengwa wakumbuke kuwa TASAF haitakuwepo siku zote, hivyo wajiwekee akiba kwa kufanya shughuli za kujipatia kipato.

Pia tuwapongeze walengwa wanaofanya vizuri kwenye matumizi ya ruzuku za TASAF na tuwakemee wale wanaotumia vibaya ruzuku hizo.

Niwatakie kila la heri katika kikao kazi hiki, kisha kusema hayo natamka rasmi kwamba kikao kimefunguliwa.

Mhe. Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe, Col. Michael M. Ngayalina (katikati), Kulia kwake ni Mhe. Venance Kigwinya, M/kiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe, na kushoto mwa picha ni Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe Ndg. Idrisa Naumanga.

Naye  M/kiti wa Halamshauri ya Wilaya ya Buhigwe, Mhe. Venance Kigwinya amemshukuru Mhe. Mkuu wa Wilaya kwa hotuba nzuri na kuahidi kuyafanyia kazi yote yaliyoagizwa. Aidha amewapongeza waelimishaji ngazi ya Jamii, Wakuu wa Idara na Vitengo, Wahe. Madiwani, Kamati ya Ulinzi na Usalama (w) kwa kuhudhuria kikao hicho.

TASAF imetusaidia sana sisi viongozi hususani katika maeneo ambayo wananchi wanamaisha duni. Tunaahidi kuendelea kutoa elimu kwa walengwa ili ruzuku hizi wazitumie vizuri hatimaye kujikwamua kwenye wimbi la umaskini wa kipato, afya, elimu n.k

Mhe. Venance Kigwinya-Mwenyekiti Halmashauri ya wilaya ya Buhigwe

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI - 04.07.2023 June 23, 2023
  • KILA KHERI DARASA LA SABA September 12, 2023
  • TANGAZO LA AJIRA - OKTOBA 2023 October 09, 2023
  • TANZIA February 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • DED BUHIGWE ATEMBELEA VITUO VYA UANDIKISHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA.

    May 05, 2025
  • MATOKEO 2024 WALIMU NA WANAFUNZI WAPONGEZWA.

    April 17, 2025
  • BABA ASKOFU EMMANUEL BWATA AITIKIA WITO WA MKURUGENZI BUHIGWE.

    April 14, 2025
  • SHEREHE YA KUWAAGA WATUMISHI NA KUWAKARIBISHA WATUMISHI BUHIGWE YAFANA.

    April 13, 2025
  • Angalia zote

Video

Hospitali ya Wilaya ya Buhigwe kuanza kutoa huduma za Afya
Video Zaidi

Kurasa Za Karibu

  • Kuhamisha Mwanafunzi
  • Tovuti ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • FFARS USER GUIDE
  • PlanRep Documentation
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • Kata Zetu
  • Wahe. Madiwani
  • BEMIS

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Bunge La Tanzania
  • Ikulu
  • Bodi Ya Manunuzi na Ugavi
  • Wizara ya Ardhi
  • Wizara ya Elimu, Sayansi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Mji Mpya wa Bwega-Ofisi za Mkurugenzi

    Postal Address: P.O.Box 443 Buhigwe

    Simu Ya Mezani: 0282988460

    Simu ya mkononi: (+255) 782 500 333

    Barua Pepe: ded@buhigwedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma
    • Mwanzo

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Buhigwe. Haki zote zimehifadhiwa