• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za ofisi |
Buhigwe District Council
Buhigwe District Council

Jamuhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Msingi Mkuu
    • Mpango Mkakati
  • Utawala
    • Muundo Wa Utawala
    • Idara
      • Utawala Na Utumishi
      • Mipango, Takwimu Na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha Na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Secondari
      • Maji
      • Mifugo Na Uvuvi
      • Ardhi Na Maliasili
      • Maendeleo Ya Jamii Na Ustawi Wa Jamii
      • Ujenzi Na Zimamoto
      • Kilimo,Umwagiliaji Na Ushirika
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi Wa Ndani
      • Habari Na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kiutalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
      • Kuonana na Mhe.Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Inayotarajiwa Kufanywa
    • Miradi Inayoendelea Kufanywa
    • New Planned Project
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Other Fomu
    • MpangoKazi
    • Baraza-Madiwani
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

RC mpya Kigoma afanya ziara yake ya kwanza wilayani Buhigwe

Posted on: September 2nd, 2020

Mkuu mpya wa Kigoma Mheshimiwa Kamishna wa Polisi Thobias Andengenye amefanya ziara ya siku mbili wilayani Buhigwe ikiwa ni mara yake ya kwanza tangu alipofika katika Mkoa wetu wa Kigoma , katika ziara yake iliyoanza tarehe 1/9/2020-2/9/2020 Mhe. Andengenye alipata fursa ya kujitambulisha kwa wananchi wa wilaya ya Buhigwe , kukagua miradi ya maendeleo, kufanya mikutano ya hadhara na kutatua kero za wananchi.

Awali akizungumza na wananchi wa kata ya Munanila Andengenye amesisitiza mambo makuu manne, kwanza Wananchi kujiunga na mfuko wa Bima ya Afya (Chf iliyoboreshwa) kwa kulipia shilingi 30000/= kwa kila kaya kwa mwaka mzima ambapo itamwezesha mwananchi kupata huduma za matibabu bure na kwamba Bima ya afya ni ufunguo wa kumuona Daktari, kupata vipimo na kuchukua dawa kuanzia ngazi ya Zahanati, Vituo vya afya na Hospitali, Pili wazazi na walezi kuhakikisha watoto wanahudhuria masomo kwani serikali ya awamu ya tano inatenga kiasi cha Bilioni 24 kila mwaka katika kutekeleza mpango wa elimu bure, Tatu ni swala la Ulinzi na Usalama; lazima kila mmoja wetu awe mlinzi wa mwenzake kwa kutoa ushirikiano kwa vyombo mbalimbali vya dola kama jeshi la Polisi. Tusifiche wahalifu tutoe taarifa za kweli siyo za fitina, Nne Tunaelekea kwenye Uchaguzi mkuu, nitoe rai kwa wananchi wote wenye sifa za kupiga kura mjitokeze kwa wingi kwenda kupiga kura ili  kumchagua kiongozi unayempenda kwa maendeleo ya Taifa letu.

Kisha hapo Mhe. Mkuu wa Mkoa alielekea eneo kinapojengwa chuo cha VETA na kuridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa chuo hicho kabla ya kukagua ujenzi wa Hospitali ya wilaya, Shule ya Msingi Mji Mpya na Jengo la ofisi ya Mkuu wa Wilaya Buhigwe, akikagua ujenzi wa bwalo la kulia chakula katika shule ya msingi Mji mpya Andengenye amesema ijengwe mifumo ya kung'amua moshi (smoke detector)na Fire extinguisher ili kuzuia hatari ya mlipuko wa moto.

Aidha akiongea na wananchi wa kata ya Munzeze Mhe. Mkuu wa Mkoa amewapongeza  wananchi kwa shughuli za maendeleo hususani kilimo cha tangawizi, "niwahakikishie tu kwamba Serikali ya awamu ya tano imewaletea nishati ya umeme ili kujenga kiwanda cha kusindika tangawizi na hivyo tuanze kuuza tangawizi iliyochakatwa".Alisema Andengenye.

Mhe. Mkuu wa Mkoa Thobias Andengenye akizungumza na wananchi wa kata ya Munzeze wakati wa ziara yake wilayani Buhigwe.

Hata hivyo Andengenye alipata fursa ya kutembelea mradi wa maji unaojengwa katika kata ya Munyegera na kushiriki uchimbaji wa mtaro wa kusafirisha maji kutoka kwenye chanzo hadi kwenye tanki la kijij.

Mhe. Andengenye akishiriki uchimbaji mtaro wa maji katika kata ya Munyegera wilayani Buhigwe wakati wa ziara yake leo.

Ziara iliendelea ambapo Mkuu wa mkoa na timu yake alielekea Shule ya sekondari Muyama na kukagua ofisi iliyojengwa kwa mradi wa EP4R na kutokuridhishwa na miundombinu ya ofisi hiyo ndipo alimwamuru Mhandisi wa Ujenzi wilaya Eng. Zacharia Ntambala kuhakikisha marekebisho  ya sakafu na marumaru yanafanyika haraka. Baada ya hapo alielekea kijiji cha Kasumo kuzungumza na wananchi kwenye mkutano wa hadhara kabla ya kuelekea kijiji cha Migongo kuwasha umeme wa REA kwa kaya 12 za mwanzo.

Kwa upande wake Bi. Agneta Kmlenga ambaye ni miongoni mwa wananchi waliopata huduma ya umeme katika kijiji cha Migongo amesema "Naishukuru sana Serikali ya awamu ya tano kwa kuniletea umeme na nitautumia kwa kufanya ujasiriamali mdogomdogo kama kutengeneza juisi na kuuza ili kujipatia kipato, nitanunua jokofu, jiko la umeme, pasi na nitauza maji baridi".

 Na mwisho kabisa Mkuu wa Mkoa  alihitimisha ziara yake katika kata ya Mugera ambapo aliongea na wananchi katika mkutano wa hadhara na kuwashukuru mamia ya wakazi waliojitokeza kumpokea.

Mhe. Mkuu wa Mkoa Kigoma akikata utepe kuashiria kuwashwa kwa umeme wa REA katika kijiji cha Migongo. Picha na Alexander Michael@Information Officer Buhigwedc

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI - 04.07.2023 June 23, 2023
  • KILA KHERI DARASA LA SABA September 12, 2023
  • TANGAZO LA AJIRA - OKTOBA 2023 October 09, 2023
  • TANZIA February 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • DED BUHIGWE ATEMBELEA VITUO VYA UANDIKISHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA.

    May 05, 2025
  • MATOKEO 2024 WALIMU NA WANAFUNZI WAPONGEZWA.

    April 17, 2025
  • BABA ASKOFU EMMANUEL BWATA AITIKIA WITO WA MKURUGENZI BUHIGWE.

    April 14, 2025
  • SHEREHE YA KUWAAGA WATUMISHI NA KUWAKARIBISHA WATUMISHI BUHIGWE YAFANA.

    April 13, 2025
  • Angalia zote

Video

Hospitali ya Wilaya ya Buhigwe kuanza kutoa huduma za Afya
Video Zaidi

Kurasa Za Karibu

  • Kuhamisha Mwanafunzi
  • Tovuti ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • FFARS USER GUIDE
  • PlanRep Documentation
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • Kata Zetu
  • Wahe. Madiwani
  • BEMIS

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Bunge La Tanzania
  • Ikulu
  • Bodi Ya Manunuzi na Ugavi
  • Wizara ya Ardhi
  • Wizara ya Elimu, Sayansi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Mji Mpya wa Bwega-Ofisi za Mkurugenzi

    Postal Address: P.O.Box 443 Buhigwe

    Simu Ya Mezani: 0282988460

    Simu ya mkononi: (+255) 782 500 333

    Barua Pepe: ded@buhigwedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma
    • Mwanzo

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Buhigwe. Haki zote zimehifadhiwa