• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za ofisi |
Buhigwe District Council
Buhigwe District Council

Jamuhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Msingi Mkuu
    • Mpango Mkakati
  • Utawala
    • Muundo Wa Utawala
    • Idara
      • Utawala Na Utumishi
      • Mipango, Takwimu Na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha Na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Secondari
      • Maji
      • Mifugo Na Uvuvi
      • Ardhi Na Maliasili
      • Maendeleo Ya Jamii Na Ustawi Wa Jamii
      • Ujenzi Na Zimamoto
      • Kilimo,Umwagiliaji Na Ushirika
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi Wa Ndani
      • Habari Na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kiutalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
      • Kuonana na Mhe.Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Inayotarajiwa Kufanywa
    • Miradi Inayoendelea Kufanywa
    • New Planned Project
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Other Fomu
    • MpangoKazi
    • Baraza-Madiwani
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

RC Andengenye: Ulinzi wa Mwanamke na Mtoto ni jukumu langu, iCHF mkombozi wa wananchi

Posted on: June 17th, 2021

Hayo yamesemwa na Mhe. ,Mkuu wa Mkoa Kigoma, Kamishna wa Polisi Thobias Andengenye wakati wa ziara yake leo wilayani Buhigwe iliyolenga kuhamasisha Jamii juu ya Ulinzi wa Mwanamke na mtoto na Kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii ulioboreshwa. Ziara hii imefanyika katika kijiji cha Nyaruboza, kata ya Muhinda, Tarafa ya Manyovu.

Akizungumza na umati wa wananchi kijijini hapo, Mhe. Mkuu wa Mkoa amesema, kulingana na utafiti, asilimia 60 ya ukatili dhidi ya watoto hutokea nyumbani na asilimia 50 hutokea shuleni ambapo wasababishi wa ukatili huo ni wazazi, walezi, ndugu na jamaa, walimu, watumishi wa shule na wanafunzi wenyewe.

Aidha unyanyasaji wa kingono; watoto 3 kati ya 10 wasichana, na mtoto 1 kati ya 7 wa kiume wamefanyiwa ukatili kabla hawajafikisha umri wa miaka 18. Unyanyasaji wa kimwili; asilimia 72 ya watoto wa kike na asilimia 71 ya watoto wa kiume wamefanyiwa ukatili kabla hawajafikisha umri wa miaka 18, Mtoto 1 kati ya 4 wamefanyiwa unyanyasaji wa kihisia kabla ya kufikisha umri wa miaka 18.

Yapo maeneo 8 ya kimkakati ambayo yatatusaidia kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto; maeneo hayo ni pamoja na;

1. Kuimarisha Uchumi wa kaya

2. Mila na Destuli

3. Mazingira salama

4. Malezi, Kuimarisha mahusiano na kuziwezesha Familia

5. Utekelezaji na Usimamizi wa sheria

6. Utoaji wa Huduma kwa waathirika wa ukatili

7. Mazingira salama shuleni na stadi za maisha

8. Uratibu, Ufuatiliaji na Tathmini

Nawaagiza wazazi na walezi kuwaandikisha shule watoto wenye ulemavu ili wapate haki ya kuendelezwa, kupata elimu na kucheza na wenzao, kitendo cha kuwafungia ndani ni kinyume cha haki za binadamu.Tuondoe dhana potofu kwamba mtoto mwenye ulemavu ni ishara ya mikosi katika familia.

Kwa upande wa Mfuko wa Afya ulioboreshwa , Rc amesema zipo huduma nyingi zitolewazo kwa Mwanachama mwenye kadi ya CHF iliyoboreshwa ikiwemo; Ushauri wa Daktari, Vipimo vya maabara, Dawa, Uangalizi, Upasuaji, Huduma za kujifungua, Huduma za rufaa, Vipimo vya picha (x-rayna ultra sound), kulazwa. Huduma hizi zinatolewa kuanzia ngazin ya Zahanati, Kituo cha Afya, Hospitali ya wilaya na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa.

Mhe. Mkuu wa Mkoa akitoa ofa ya kitambulisho cha Mfuko wa Bima ya Afya ulioboreshwa kwa Bi. Vaileth Kizanye.

Akisoma risala mbele ya Mgeni rasmi, Mganga Mkuu wa wilaya ya Buhigwe Dkt. Julius Nyasongo, amesema wananchi wanaendelea kujitokeza kujiunga na Mfuko wa CHF iliyoboreshwa na elimu ya kupinga ukatili dhidi ya mwanamke na mtoto inaendelea kutolewa kupitia kamati za MTAKUWWA ngazi ya Wilaya, Kata na Vijiji.

Dkt. Julius Nyasongo akisoma risala kwa Mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa Kigoma wakati wa ziara kijijini Nyaruboza tarehe 17/06/2021.

Kwa upande wake Mhe. Mkuu wa wilaya ya Buhigwe Col. Michael M. Ngayalina alitoa ofa ya shilingi elfu tano kwa kila mwanachama mpya anayejiunga na CHF iliyoboreshwa kabla ya Mhe. Diwani wa katay hiyo kuhitimisha kwa kutoa ofa ya vitambulisho viwili vya mfuko wa CHF iliyoboreshwa.

Imetolewa na;

Idara ya TEHAMA, 

Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji (w) Mji wa Bwega,

P.O.BOX 443

 Buhigwe

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI - 04.07.2023 June 23, 2023
  • KILA KHERI DARASA LA SABA September 12, 2023
  • TANGAZO LA AJIRA - OKTOBA 2023 October 09, 2023
  • TANZIA February 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • DED BUHIGWE ATEMBELEA VITUO VYA UANDIKISHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA.

    May 05, 2025
  • MATOKEO 2024 WALIMU NA WANAFUNZI WAPONGEZWA.

    April 17, 2025
  • BABA ASKOFU EMMANUEL BWATA AITIKIA WITO WA MKURUGENZI BUHIGWE.

    April 14, 2025
  • SHEREHE YA KUWAAGA WATUMISHI NA KUWAKARIBISHA WATUMISHI BUHIGWE YAFANA.

    April 13, 2025
  • Angalia zote

Video

Hospitali ya Wilaya ya Buhigwe kuanza kutoa huduma za Afya
Video Zaidi

Kurasa Za Karibu

  • Kuhamisha Mwanafunzi
  • Tovuti ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • FFARS USER GUIDE
  • PlanRep Documentation
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • Kata Zetu
  • Wahe. Madiwani
  • BEMIS

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Bunge La Tanzania
  • Ikulu
  • Bodi Ya Manunuzi na Ugavi
  • Wizara ya Ardhi
  • Wizara ya Elimu, Sayansi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Mji Mpya wa Bwega-Ofisi za Mkurugenzi

    Postal Address: P.O.Box 443 Buhigwe

    Simu Ya Mezani: 0282988460

    Simu ya mkononi: (+255) 782 500 333

    Barua Pepe: ded@buhigwedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma
    • Mwanzo

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Buhigwe. Haki zote zimehifadhiwa