• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za ofisi |
Buhigwe District Council
Buhigwe District Council

Jamuhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Msingi Mkuu
    • Mpango Mkakati
  • Utawala
    • Muundo Wa Utawala
    • Idara
      • Utawala Na Utumishi
      • Mipango, Takwimu Na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha Na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Secondari
      • Maji
      • Mifugo Na Uvuvi
      • Ardhi Na Maliasili
      • Maendeleo Ya Jamii Na Ustawi Wa Jamii
      • Ujenzi Na Zimamoto
      • Kilimo,Umwagiliaji Na Ushirika
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi Wa Ndani
      • Habari Na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kiutalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
      • Kuonana na Mhe.Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Inayotarajiwa Kufanywa
    • Miradi Inayoendelea Kufanywa
    • New Planned Project
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Other Fomu
    • MpangoKazi
    • Baraza-Madiwani
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

RC Andengenie akagua miradi ya UN Kigoma Joint Programme-Buhigwe

Posted on: June 1st, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe. Kamishna wa Polisi Thobias Andengenie hivi karibuni amefanya ziara ya kukagua miradi ya UN Kigoma JOINT PROGRAMME iliyotekelezwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe kwa kutembelea kata nne (4) ambapo miradi hiyo imejengwa. Kata hizo ni pamoja na KINAZI, JANDA, MUYAMA na BUHIGWE.

Katika kata za Kinazi na Janda, amekagua viwanda vidogo vya kukamua Mawese vilivyojengwa kwa ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania na Kituo cha Biashara Duniani (ITC) kupitia mradi wa pamoja wa Umoja wa Mataifa Mkoa wa Kigoma (UN-KJP).

Mhe. Andengenie, amewahimiza wananchi kuongeza uzalishaji wa mafuta ya mawese ili viwanda hivyo vilete tija katika jamii inayowazunguka, kujenga uzio kuzunguka eneo la viwanda, kuandaa vifungashio kwakuwa vifungashio ndio kivutio cha macho ya wateja, kuandaa LEBO itakayotambulisha biashara yao ya mafuta ya mawese.

"Wito wangu kwa Afisa Biashara Mkoa na Maafisa Biashara wote, tuwe na duka letu ngazi ya mkoa linalotambulisha bidhaa zetu za mawese na endapo uzalishaji utaongezeka basi tutapanua soko kwa kufungua maduka mengine nje ya mkoa wetu wa Kigoma" Alisema Andengenie.

Mwisho aliwapatia akina mama zawadi ya Shilingi Milioni Moja baada ya kuvutiwa na usimamizi katika kuendesha viwanda hivyo.

Kwa upande wao, akina mama, walimshukuru sana Mhe. Mkuu wa Mkoa kwa kufanya ziara yake katani hapo na kumpatia zawadi ya Jogoo mwenye thamani ya Shilingi Elfu ishirini.

Akina Mama katika Kata ya Janda wakimkabidhi zawadi ya Jogoo Mhe. Mkuu wa Mkoa Kigoma, wakati wa ziara yake katani hapo.

Akiwa kata ya Buhigwe, Mhe. Andengenie, alitembelea jengo la Vijana ambalo pia limejengwa kwa hisani ya UN-KJP na kuzungumza na watumishi wa ummma na baadhi ya vijana waliohudhuria ziara hiyo.

Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii, Ndg. Christopher Kajange akisoma taarifa ya mradi wa Jengo la vijana wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa Kigoma.

Ziara ilihitimishwa kwa kutembelea Soko la Muyama, ambapo ujenzi unaendelea na utarajia kukamilika mwezi Julai, 2021.

Soko la Muyama katika hatua ya kupandisha ukuta.

Imetolewa na Kitengo cha Tehama, Ofisi ya Mkurugenzi, Mji wa Bwega, P.o.box 443,-Buhigwe.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI - 04.07.2023 June 23, 2023
  • KILA KHERI DARASA LA SABA September 12, 2023
  • TANGAZO LA AJIRA - OKTOBA 2023 October 09, 2023
  • TANZIA February 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • DED BUHIGWE ATEMBELEA VITUO VYA UANDIKISHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA.

    May 05, 2025
  • MATOKEO 2024 WALIMU NA WANAFUNZI WAPONGEZWA.

    April 17, 2025
  • BABA ASKOFU EMMANUEL BWATA AITIKIA WITO WA MKURUGENZI BUHIGWE.

    April 14, 2025
  • SHEREHE YA KUWAAGA WATUMISHI NA KUWAKARIBISHA WATUMISHI BUHIGWE YAFANA.

    April 13, 2025
  • Angalia zote

Video

Hospitali ya Wilaya ya Buhigwe kuanza kutoa huduma za Afya
Video Zaidi

Kurasa Za Karibu

  • Kuhamisha Mwanafunzi
  • Tovuti ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • FFARS USER GUIDE
  • PlanRep Documentation
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • Kata Zetu
  • Wahe. Madiwani
  • BEMIS

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Bunge La Tanzania
  • Ikulu
  • Bodi Ya Manunuzi na Ugavi
  • Wizara ya Ardhi
  • Wizara ya Elimu, Sayansi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Mji Mpya wa Bwega-Ofisi za Mkurugenzi

    Postal Address: P.O.Box 443 Buhigwe

    Simu Ya Mezani: 0282988460

    Simu ya mkononi: (+255) 782 500 333

    Barua Pepe: ded@buhigwedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma
    • Mwanzo

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Buhigwe. Haki zote zimehifadhiwa