• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za ofisi |
Buhigwe District Council
Buhigwe District Council

Jamuhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Msingi Mkuu
    • Mpango Mkakati
  • Utawala
    • Muundo Wa Utawala
    • Idara
      • Utawala Na Utumishi
      • Mipango, Takwimu Na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha Na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Secondari
      • Maji
      • Mifugo Na Uvuvi
      • Ardhi Na Maliasili
      • Maendeleo Ya Jamii Na Ustawi Wa Jamii
      • Ujenzi Na Zimamoto
      • Kilimo,Umwagiliaji Na Ushirika
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi Wa Ndani
      • Habari Na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kiutalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
      • Kuonana na Mhe.Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Inayotarajiwa Kufanywa
    • Miradi Inayoendelea Kufanywa
    • New Planned Project
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Other Fomu
    • MpangoKazi
    • Baraza-Madiwani
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO ASHIRIKI UJENZI WA ZAHANATI NA KIWANDA – BUHIGWE

Posted on: July 14th, 2021
  • Apongeza juhudi za wananchi, halmshauri na uongozi wa wilaya
  • Achangia 500,000 Ujenzi wa Zahanati na 100,000 Kiwanda cha MAWESE cha akina mama
  • Aahidi serikali kutia mkono ukamilishaji Zahanati
  • Asisitiza utunzaji wa Nyaraka zote za ujenzi kukwepa ubadhirifu
  • Awataka wanachi kujikinga na UVIKO 19
  • Awataka maafisa maendeleo Kutoka ofisini kuwatembelea wananchi, pia atoe wito waendelee kukuza ari ya wanachi kujiletea maendeleo kwa rasilimali zinazowazunguka
  • Akemea vikali Unyanyasaji na ukatili wa kijinsia kwa kina mama na Watoto
  • Awataka akina mama kutokukaa kimya kata vitendo viovu, vya kiuonevu na dhuluma juu yao
  • Awataka Vijana kuchangamkia Fursa ya Asilimia 4 kubuni miradi
  • Amwaga sifa kede kede kwa Makamu war ais Mhe. DKT Mpango na kwa Mhe. Rais Samia
  • Bima ya afya kwa wananchi yasisitizwa.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na Watoto Mhe. Mwanaid Ali Khamis (MB) ametembelea na kushiriki ujenzi wa Zahanati ya Kibuye Kata ya BUKUBA wilayani Buhigwe Pamoja na kujionea maendeleo ya Ujenzi wa  Kiwanda kidogo cha kuchakata zao la chikichi (Uzalishaji wa mafuta ya MAWESE) cha akina mama cha NYAMUNINYA.

Awali katika kushiriki zoezi la ujenzi wa Zahanati ya Kibuye, akisoma taarifa ya ujenzi wa zahanati hiyo ambayo imefikia hatua ya Linta, Mtendaji wa Kijiji hicho alisema Gharama za ujenzi wa Zahanati hiyo hadi kufikia hatua hiyo ni Tsh 14,238,600 ambapo fedha hizo ni nguvu ya wananchi na halmahsauri ya wilaya. Aliongeza kuwa jumla ya gharama za ujenzi huo hadi kukamilika ni Tsh 65,000,000 na kumuomba Mh Naibu kuchangia na kutia mkazo kiasi kinachobaki kupatikana kutoka serikalini ili kukamilisha boma la zahanati hiyo. Taarifa ya mtendaji huyo iliongeza kuwa ari ya wananchi ilikuja baada ya kupata adha za kutembea umbali mrefu kufuata huduma ya afya kwenye kata ya Jirani ya Janda.

Katika kujibu taarifa ya ujenzi Mhe. Naibu Waziri alichangia papo hapo Tsh Laki 5 na kuahidi kufikisha ombi la fedha zinazobaki kwa serikali. Aliendelea kwa kuwashukuru wananchi kwa moyo wa kujitolea na kusisitiza kuendelea kutumia rasilimali zinazowazunguka kutimiza malengo ya maendeleo.

Katika kuhitimisha hotuba yake eneo la kwanza akishiriki ujenzi wa Zahanati alisisitiza wanachi kuendelea kuchukua Tahadhari dhidi ya Ugonjwa wa UVIKO 19 na kukemea vikali unyanyasaji wa kijinsia kwa akina mama na Watoto na kuwataka kutokukaa kimya pindi matendo hayo yanapofanywa juu yao au kwa Watoto wao.

Awali kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri, Mkuu wa wilaya hiyo Mhe. Kanali Michael Ngayalina alisisitiza kuwa bima Afya ni muhimu na ametia hamasa kwa kumuongezea Tsh 5,000 kwa kila mwananchi atakayehitaji bima ya afya. Katika hotuba yake Naibu Waziri aliungana na Mkuu wa wilaya hiyo kusisitiza kuwa magonjwa hayana hodi huja wakati wowote hivyo bima ya Afya ni mkombozi sahihi.

Upande mwingine wakati akijionea ujenzi wa Kiwanda cha Kuchakata mazao ya Chikichi  (Kuzalisha mafuta ya MAWESE)-cha Akina mama Nyamuninya, Naibu Waziri amekipongeza kikundi hicho, uongozi wa Kijiji, halmashauri na wadau wa maendeleo kama ITC na SIDO (kupitia mradi wa Pamoja wa Kigoma (KJP) kwa ubunifu wanaofanya kuongeza viwanda hasa vinavyomilikiwa na vikundi vya akina mama.

Awali akisoma taarifa ya ujenzi wa kiwanda hicho kwa niaba ya wanakikundi wa Nyamuninya Mtendaji wa Kijiji alisema Gharama za ujenzi huo ni Tsh 57,641,620 ambapo Mchango wa ITC na SIDO kupitia mradi wa Pamoja KJP ni Tsh 56,525,000/= na kikundi kilichangia 1,116,620. Katika kutia chachu ya ykamilishaji Naibu Waziri alikipa kikundi Tsh Laki 1

Katika kuhutimisha hotuba yake Naibu Waziri alipigilia msumari kwa kuwataka wanawake kutokaa kimya kwa aina yoyote ya unyanyasaji wa kijinsia kwao au kwa Watoto wao na kuwataka kuwa tayari kutoa Ushahidi pale wanapohitajika

Naibu Waziri pia aliwataka vijana kuchangamkia asilimia nne za halmasahuri za vijana kujiletea maendeleo kwa kuanzisha miradi kukuza kipato

Awali Mwenyekiti wa CCM wilaya alipopewa nafasi kabla ya Naibu Waziri kuhotubia alimshukuru na kutuma salamu kwa Mhe. Makamu wa Rais na Mhe. Rais huku kilio cha watumishi wilayani hapo akimtwika Naibu Waziri kulitizama kwa jicho la tatu.

Mwisho Diwani wa kata hiyo Alimshukuru Waziri kwa wito na moyo kwa yote aliyofanya na kusisitiza kuwa shughuli za maendeleo katani kwake zinaenda kwa kasi na kumkaribisha tena Bukuba.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI - 04.07.2023 June 23, 2023
  • KILA KHERI DARASA LA SABA September 12, 2023
  • TANGAZO LA AJIRA - OKTOBA 2023 October 09, 2023
  • TANZIA February 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • DED BUHIGWE ATEMBELEA VITUO VYA UANDIKISHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA.

    May 05, 2025
  • MATOKEO 2024 WALIMU NA WANAFUNZI WAPONGEZWA.

    April 17, 2025
  • BABA ASKOFU EMMANUEL BWATA AITIKIA WITO WA MKURUGENZI BUHIGWE.

    April 14, 2025
  • SHEREHE YA KUWAAGA WATUMISHI NA KUWAKARIBISHA WATUMISHI BUHIGWE YAFANA.

    April 13, 2025
  • Angalia zote

Video

Hospitali ya Wilaya ya Buhigwe kuanza kutoa huduma za Afya
Video Zaidi

Kurasa Za Karibu

  • Kuhamisha Mwanafunzi
  • Tovuti ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • FFARS USER GUIDE
  • PlanRep Documentation
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • Kata Zetu
  • Wahe. Madiwani
  • BEMIS

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Bunge La Tanzania
  • Ikulu
  • Bodi Ya Manunuzi na Ugavi
  • Wizara ya Ardhi
  • Wizara ya Elimu, Sayansi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Mji Mpya wa Bwega-Ofisi za Mkurugenzi

    Postal Address: P.O.Box 443 Buhigwe

    Simu Ya Mezani: 0282988460

    Simu ya mkononi: (+255) 782 500 333

    Barua Pepe: ded@buhigwedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma
    • Mwanzo

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Buhigwe. Haki zote zimehifadhiwa