• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za ofisi |
Buhigwe District Council
Buhigwe District Council

Jamuhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Msingi Mkuu
    • Mpango Mkakati
  • Utawala
    • Muundo Wa Utawala
    • Idara
      • Utawala Na Utumishi
      • Mipango, Takwimu Na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha Na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Secondari
      • Maji
      • Mifugo Na Uvuvi
      • Ardhi Na Maliasili
      • Maendeleo Ya Jamii Na Ustawi Wa Jamii
      • Ujenzi Na Zimamoto
      • Kilimo,Umwagiliaji Na Ushirika
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi Wa Ndani
      • Habari Na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kiutalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
      • Kuonana na Mhe.Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Inayotarajiwa Kufanywa
    • Miradi Inayoendelea Kufanywa
    • New Planned Project
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Other Fomu
    • MpangoKazi
    • Baraza-Madiwani
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

MITI MILIONI 2 KUPANDWA BUHIGWE

Posted on: November 21st, 2023


Mhe. Col. Michael Ngayalina, Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe ameongoza zoezi la upandaji miti kwenye eneo inapojengwa Shule Mpya ya Sekondari Biharu, katani Biharu Wilayani humo ambapo katika kutekeleza dhana ya utunzaji wa Mazingira Mkuu huyo wa Wilaya amewataka wananchi kuridhisha tabia ya utunzaji mazingira kwa kizazi kijacho kwa kuwa kutunza mazingira ni kutunza Maisha

Mkurugenzi wa Programu ya Tuungane ambayo imejikita katika Utunzaji wa Mazingira kupitia Utunzaji na Upandaji Miti, Ndg. Lukindo Hiza ameshukuru namna ambavyo wananchi wameipokea Program hiyo na kuonesha Ushirikiano katika kufikia Lengo la Buhigwe ya Kijani yenye Uoto wa Asili.

Awali Ndg. Alphonce Haule, Kaimu mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe amesema wameazimia kwenye Baraza la Madiwani kuwa kila Kata kuwa na Shamba la Miti ili kuenedeleza kuenzi dhana ya Utunzaji wa Mazingira kwa upandaji miti kwa Vitendo.

Ndg. Utefta Mahega, Katibu Tawala wa Wilaya hiyo ameshukuru namna Zoezi na Program hiyo inavyoendeshwa ili kubadili Buhigwe ambayo uharibifu wa Mazingira nii Mkubwa hivyo kutishia kizazi cha sasa na kijacho.

Mhe. Felix Kavejuru, Mbunge wa Jimbo la Buhigwe akiwasilisha Salamu za Mhe Samia Suluhu Hassan, amewataka wananchi kutumia Mvua zinazoendelea kunyesha kulima kikamilifu ili kuepukana na majanga ya njaa ila wazitumie kuzalisha ili kupata Chakula cha kutosha na kujiongezea kipato kwao na kwa Halamshauri.

Kabla ya zoezi la Upandaji Miti kwenye eneo hilo, uongozi wa Wilaya walitembelea na kukagua vitalu vyenye miche Takribani Milioni 2 ya aina mbali mbali hasa yenye kulinda na kutunza maji ambapo vitalu hivyo vinatunzwa na kikundi cha Tuungane ambacho baada ya kukuza miti hiyo huigawa Bure kwa wananchi ili wapande kwenye maeneo yao Pamoja na taasisi.

Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi wa Wilaya hawakuwa nyuma kushiriki zoezi hilo ambapo kupitia Mwenyekiti wao Ndg. Erneo Dyagula wameshukuru namna ambavyo wananchi wameendelea kumuunga Mkono Mhe. Rais Samia kwa Vitendo na kuwataka waendelee kujitokeza kila shughuli ya Maendeleo inapofanyika ili kufikia Buhigwe inayotajwa na Ilani.

Wilaya ya Buhigwe ni miongoni mwa Wilaya zenye Mvua nyingi lakini kutokana na uharibifu wa Mazingira maeneo mengi yamebaki na nyasi fupi na vichaka tofauti na awali ambapo miti ya asili ilitamalaki kila mahali ambapo sasa Juhudi za makusudi za kila mmoja zinahitajika, akiongeza kwenye Hotuba yake Mhe Ngayalina amewasihi wananchi kuacha tabia ya Uchomaji holela wa Miti

Jumla ya Miti 1000 imepandwa kwenye eneo hilo kama ishara ya kuendelea kutia shime wananchi kuendeleza dhana ya Utunzaji wa mazingira kwa Upandaji Miti ambapo zoezi hilo limeongozwa na Mhe. Ngayalina ambaye  amekuwa Kielelezo katika kuhakikisha dhana ya Utunzaji mazingira inafanywa kwa vitendo wilayani hapo ambapo kila mwaka wamedhamiria kupanda Miche mipya Takribani Milioni Mbili hadi Tatu

Program ya Tuungane inatekelezwa Wilayani Humo ikiwa na Jumla ya Vitalu Viwili Wilayani Humo vyenye Jumla ya Miche 2,080,000.

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI - 04.07.2023 June 23, 2023
  • KILA KHERI DARASA LA SABA September 12, 2023
  • TANGAZO LA AJIRA - OKTOBA 2023 October 09, 2023
  • TANZIA February 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • DED BUHIGWE ATEMBELEA VITUO VYA UANDIKISHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA.

    May 05, 2025
  • MATOKEO 2024 WALIMU NA WANAFUNZI WAPONGEZWA.

    April 17, 2025
  • BABA ASKOFU EMMANUEL BWATA AITIKIA WITO WA MKURUGENZI BUHIGWE.

    April 14, 2025
  • SHEREHE YA KUWAAGA WATUMISHI NA KUWAKARIBISHA WATUMISHI BUHIGWE YAFANA.

    April 13, 2025
  • Angalia zote

Video

Hospitali ya Wilaya ya Buhigwe kuanza kutoa huduma za Afya
Video Zaidi

Kurasa Za Karibu

  • Kuhamisha Mwanafunzi
  • Tovuti ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • FFARS USER GUIDE
  • PlanRep Documentation
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • Kata Zetu
  • Wahe. Madiwani
  • BEMIS

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Bunge La Tanzania
  • Ikulu
  • Bodi Ya Manunuzi na Ugavi
  • Wizara ya Ardhi
  • Wizara ya Elimu, Sayansi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Mji Mpya wa Bwega-Ofisi za Mkurugenzi

    Postal Address: P.O.Box 443 Buhigwe

    Simu Ya Mezani: 0282988460

    Simu ya mkononi: (+255) 782 500 333

    Barua Pepe: ded@buhigwedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma
    • Mwanzo

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Buhigwe. Haki zote zimehifadhiwa