• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za ofisi |
Buhigwe District Council
Buhigwe District Council

Jamuhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Msingi Mkuu
    • Mpango Mkakati
  • Utawala
    • Muundo Wa Utawala
    • Idara
      • Utawala Na Utumishi
      • Mipango, Takwimu Na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha Na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Secondari
      • Maji
      • Mifugo Na Uvuvi
      • Ardhi Na Maliasili
      • Maendeleo Ya Jamii Na Ustawi Wa Jamii
      • Ujenzi Na Zimamoto
      • Kilimo,Umwagiliaji Na Ushirika
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi Wa Ndani
      • Habari Na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kiutalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
      • Kuonana na Mhe.Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Inayotarajiwa Kufanywa
    • Miradi Inayoendelea Kufanywa
    • New Planned Project
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Other Fomu
    • MpangoKazi
    • Baraza-Madiwani
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

UONGOZI WA H/W BUHIGWE WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO-MUFINDI

Posted on: August 30th, 2023

Uongozi kutoka Halmashauri ya Wilaya Buhigwe Mkoani Kigoma Ukiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe Mhe. Kanali Michael Ngayalina, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Buhigwe Mhe. Alphonce Haule, Mwenyekiti wa Halmashauri  ya Wilaya ya Buhigwe Ndg. Venance Kigwinya pamoja na Baraza la Madiwani wamefanya ziara katika Wilaya ya Mufindi shamba la miti Saohill na Kupokelewa na Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe. Dkt Linda P Salekwa ili  kujifunza shughuli za uhifadhi wa misitu na zinavyofanyika katika shamba hilo.

Akizungumza katika ziara hiyo Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe Kanali Ngalina ameanza kutoa shukrani zake kwa Serikali ya awamu ya sita kwa kuendeleza uwekezaji kwa Wakala wa Huduma za Misitu ‘TFS’ Tanzania ili kuendeleza uhifadhi na kuchangia katika upatikanaji wa mapato yatokanayo na mazao mbalimbali ya misitu.

 

Amesema kuwa ziara hiyo imedhaminiwa na Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe kwa kushirikiana na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania-TFS ili kuhakikisha wanafanikisha lengo la kuja kujifunza shughuli za uhifadhi.

"Kwa namna ya Pekee nipende kumshukuru Kamishna wa Uhifadhi Prof. Dos Santos Silayo ambaye alitembelea Wilaya yetu na baada ya kuona chamgamoto tunazozipata alitualika ili tuweze kufanya ziara hii pamoja na Waheshimiwa madiwani" amesema.

Ameongeza kuwa katika wilaya ya Buhigwe ina hali ya hewa inafanana na na eneo la wilaya ya Mufindi lakini pia wana maeneo mengi ya wazi ‘vipara’ ambayo yanafaa kupandwa miti na kuendeleza dhana ya Uhifadhi na kupata mapato kama ilivo huku.


Kwa Upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Buhigwe Alphonce Haule ameipongeza TFS kwa kazi inayofanya na kusema wamejifunza vitu vingi kutoka Saohill ikiwemo uhifadhi wa misitu na utunzaji wa mazingira.

" Tumepita kwenye vitalu vya kuzalisha miche

na tumeona jinsi inavyoandaliwa na tumegundua kwamba sisi kama Halmshauri ya Buhigwe tunayo nafasi ya kuanzisha shamba letu ambalo litakuwa ni mojawapo ya chanzo cha mapato"

Aidha ameongeza kuwa kama halmashauri wanayo nafasi ya kukaa pamoja na uongozi wa TFS Buhigwe na kuona uwezekano wa kuwaongezea eneo lingine sababu eneo lililopo kwa sasa ni dogo.

Mhe. Elesi Elia Gwoma ni Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe kwa upande wake anaipongeza na TFS kwa jazi inayofanyika ya Uhifadhi. Amesema kama halmshauri wamepata elimu kubwa ambayo itawachagiza na wao kufanya uhaifadhi kama walivyoona kutoka katika Shamba la miti Saohill. Ameongeza kuwa huko Buhigwe hata wao wanayo misiti lakini hawapo kwenye hatua kama waliyojifunza hapa hivyo nao watafanya juhudi ili kufika juu zaidi.

Naye Hassan Katura Diwani kata ya Kilelema amesema kuwa wao kama wadau wa mazingira watakuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha mazingira yanatunzwa na kusisitiza uhifadhi wa misitu kwa manufaa ya kizazi kilichopo na hata cha baadae.

" Ziara hii ni zaidi ya Shule kwetu, hivyo madiwani kama wadau wa misitu pia naamini watakwenda kuboresha mazingira wanayoyaongoza" amesema.

Katika Ziara hiyo Wageni hao waliongozwa na Mhifadhi Mkuu wa Shamba la Miti Saohill PCO Tebby Yoramu akiambatana na Mhifadhi Msaidizi  SCO Said Singano, Mhifadhi  kutoka Shamba la miti Bihigwe, Mhifadhi wa tarafa ya Kwanza pamoja na Afisa Maliasili kwa Halmashauri ya Wilaya ya Mufundi Gilbert Ngailo.

Ziara hiyo iliendelea kwa Siku ya Pili ya Tarehe 29.08.2023 kwa Wah. Madiwani na uongoiz kutembelea Viwanda vitatu vinavyozalisha thamani na vitu kutokana na malighafi za Miti kama Mkaa mbdala, Venia, Fenicha nk na baadae walitembelea Eneo unakofanywa utafiti wa Uvunaji wa Utovu wa Miti hiyo kabla ya Kuvunwa

Ziara hiyo ilihitimishwa kwa kupata mlo wa Pamoja ambapo mwisho PCO aliwashukuru na kuwakaribisha tena ana kwa niaba ya Mhe. Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe, Mhe. Venance Kigwinya ambaye ni Mwenyekiti wa Halmashauri alitoa shukrani kwa kuwakaribisha Menejimenti ya Saohill kuja Buhigwe huku akisistiza kufanya kwa vitendo mazuri waliyopata hapo.

 

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI - 04.07.2023 June 23, 2023
  • KILA KHERI DARASA LA SABA September 12, 2023
  • TANGAZO LA AJIRA - OKTOBA 2023 October 09, 2023
  • TANZIA February 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • DED BUHIGWE ATEMBELEA VITUO VYA UANDIKISHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA.

    May 05, 2025
  • MATOKEO 2024 WALIMU NA WANAFUNZI WAPONGEZWA.

    April 17, 2025
  • BABA ASKOFU EMMANUEL BWATA AITIKIA WITO WA MKURUGENZI BUHIGWE.

    April 14, 2025
  • SHEREHE YA KUWAAGA WATUMISHI NA KUWAKARIBISHA WATUMISHI BUHIGWE YAFANA.

    April 13, 2025
  • Angalia zote

Video

Hospitali ya Wilaya ya Buhigwe kuanza kutoa huduma za Afya
Video Zaidi

Kurasa Za Karibu

  • Kuhamisha Mwanafunzi
  • Tovuti ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • FFARS USER GUIDE
  • PlanRep Documentation
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • Kata Zetu
  • Wahe. Madiwani
  • BEMIS

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Bunge La Tanzania
  • Ikulu
  • Bodi Ya Manunuzi na Ugavi
  • Wizara ya Ardhi
  • Wizara ya Elimu, Sayansi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Mji Mpya wa Bwega-Ofisi za Mkurugenzi

    Postal Address: P.O.Box 443 Buhigwe

    Simu Ya Mezani: 0282988460

    Simu ya mkononi: (+255) 782 500 333

    Barua Pepe: ded@buhigwedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma
    • Mwanzo

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Buhigwe. Haki zote zimehifadhiwa