• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za ofisi |
Buhigwe District Council
Buhigwe District Council

Jamuhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Msingi Mkuu
    • Mpango Mkakati
  • Utawala
    • Muundo Wa Utawala
    • Idara
      • Utawala Na Utumishi
      • Mipango, Takwimu Na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha Na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Secondari
      • Maji
      • Mifugo Na Uvuvi
      • Ardhi Na Maliasili
      • Maendeleo Ya Jamii Na Ustawi Wa Jamii
      • Ujenzi Na Zimamoto
      • Kilimo,Umwagiliaji Na Ushirika
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi Wa Ndani
      • Habari Na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kiutalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
      • Kuonana na Mhe.Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Inayotarajiwa Kufanywa
    • Miradi Inayoendelea Kufanywa
    • New Planned Project
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Other Fomu
    • MpangoKazi
    • Baraza-Madiwani
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Ukatili wa Wanawake na Watoto Buhigwe sasa basi

Posted on: September 9th, 2020

Hayo yamesemwa leo katika kikao kazi cha Kamati ya Ulinzi na Usalama wa wanawake na watoto (MTAKUWWA)ngazi ya mkoa kilichofanyika ukumbi wa Hospitali ya wilaya ya Buhigwe majira ya saa 3 asubuhi.

Awali akisoma taarifa ya utekelezaji wa kamati ya ulinzi na usalama wa wanawake na watoto ngazi ya wilaya, Afisa Ustawi wa Jamii (w) Bwana Petro Mbwanji amesema kamati inaendelea kuhakikisha hatua kali za kisheria zinachukuliwa dhidi ya watuhumiwa wa vitendo vya ukatili wa wanawake na watoto sanjari na kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu ukatili wa wanawake na watoto na athari zake.

Aidha kamati ya MTAKUWWA (w) imetoa mafunzo kwa kamati za ulinzi na usalama wa wanawake na watoto ngazi za kata na vijiji vyote 44 vya wilaya ya Buhigwe, hata hivyo yapo mashauri ambayo yameondolewa mahakamani na mengine watuhumiwa wamehukumiwa jela.

Kwa upande wake Kaimu Afisa Elimu Mkoa Bw. Jonas Joas akijibu taarifa ya utekelezaji iliyowasilishwa na Afisa Ustawi wa Jamii (w) amesema pamoja na majukumu ya kamati hiyo ni vizuri kuhakikisha kwamba watoto wote wenye umri wa kwenda shule na walioko shule wanahudhuria masomo bila kubughudhiwa wala kuwa watoro na walau kuwe na mlo mmoja tena wenye viazi lishe shuleni . Joas aliendelea kusisitiza juu ya clubs za watoto shuleni kwamba zinapaswa kuwa na tija ili zitusaidie kuibua vitendo vya ukatili, mojawapo ya club ilyoanzishwa na mradi wa EQUIP Tanzania ni "JUU club" yaani Jiamini uwezo unao. Pia kamati ijikite kwenye upimaji wa mimba kwa watoto wa kike shuleni na kupunguza masoko ya usiku hasa kwa watoto wa kike ambao ndio wahanga wakubwa.

Naye kaimu Katibu Tawala Mkoa Mhe.Moses D. Msuluzya ametoa wiki mbili kwa  kamati ya MTAKUWWA (W) kuwatafuta wazazi na watoto ambao ni watoro ili kutambua sababu za kutokuhudhuria masomo na ni hatua gani zimechukuliwa dhidi yao. Pia viongozi wa dini msihamasishe suluhu dhidi ya vitendo vya ukatili bali kemeeni waumini wajiepushe na ukatili wa aina yoyote kwakuwa sheria haijakaa kimya.

Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt. Simon Chacha naye hakubaki nyuma kwa kushauri kuwepo kwa jengo la" One Stop Center" ili kuharakisha uamzi wa vitendo vya ukatili kwakuwa kesi nyingi za ukatili zinaishia ngazi ya jamii kiholela, pia kamati ya MTAKUWWA (W) hakikisheni swala la utumikishwaji wa watoto katika maeneo mbalimbali kama mashambani na maeneo ya ufyatuaji tofali yanakomeshwa na wahusika wanachukuliwa hatua za kisheria.

Aidha Hakimu Mkazi wa Mkoa Kigoma Mhe. Gadiel Mariki ameshauri waongezwe waendesha mashataka na OCCID(W) kwenye kamati ya MTAKUWWA na shauri l isichukue muda mrefu kufanyiwa uamzi ndipo matukio ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto yatakoma.

Naye Afisa Maendeleo ya Jamii Mkoa Kigoma amesema elimu ya vikundi vya wanawake na vijana iendelee kutolewa ili walengwa wanufaike na pesa inayotolewa na serikali.

Hata hivyo Mkurugenzi Mtendaji (w) Buhigwe ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya MTAKUWWA ngazi ya wilaya amewashukuru kamati ya MTAKUWWA ngazi ya Mkoa na kuahdi kuyafanyia kazi yote yaliyoshauriwa lengo likiwa ni kutokomeza ukatili kwa wanawake na watoto.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI - 04.07.2023 June 23, 2023
  • KILA KHERI DARASA LA SABA September 12, 2023
  • TANGAZO LA AJIRA - OKTOBA 2023 October 09, 2023
  • TANZIA February 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • DED BUHIGWE ATEMBELEA VITUO VYA UANDIKISHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA.

    May 05, 2025
  • MATOKEO 2024 WALIMU NA WANAFUNZI WAPONGEZWA.

    April 17, 2025
  • BABA ASKOFU EMMANUEL BWATA AITIKIA WITO WA MKURUGENZI BUHIGWE.

    April 14, 2025
  • SHEREHE YA KUWAAGA WATUMISHI NA KUWAKARIBISHA WATUMISHI BUHIGWE YAFANA.

    April 13, 2025
  • Angalia zote

Video

Hospitali ya Wilaya ya Buhigwe kuanza kutoa huduma za Afya
Video Zaidi

Kurasa Za Karibu

  • Kuhamisha Mwanafunzi
  • Tovuti ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • FFARS USER GUIDE
  • PlanRep Documentation
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • Kata Zetu
  • Wahe. Madiwani
  • BEMIS

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Bunge La Tanzania
  • Ikulu
  • Bodi Ya Manunuzi na Ugavi
  • Wizara ya Ardhi
  • Wizara ya Elimu, Sayansi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Mji Mpya wa Bwega-Ofisi za Mkurugenzi

    Postal Address: P.O.Box 443 Buhigwe

    Simu Ya Mezani: 0282988460

    Simu ya mkononi: (+255) 782 500 333

    Barua Pepe: ded@buhigwedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma
    • Mwanzo

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Buhigwe. Haki zote zimehifadhiwa