katibu Tawala Mkoa wa Kigoma Mh Hassan Rugwa amewataka Wauguzi na wakunga mkoani hapa kufanya kazi kwa kuzingatia kanuni na maadili ya taaluma yao.
Ametoa wito huo leo tarehe 12 May 2025 wakati akizungumza katika maadhimisho ya siku ya wauguzi duniani ambayo kwa mkoa wa kigoma yamefanyika katika kijiji cha Songambele kata ya Munyegera wilayani Buhigwe.
Aidha ameongezea kuwa serikali imeendelea kuboresha miundombinu mbalimbali ya afya katika mkoa wa Kigoma pamoja na kuweka mikakati ya kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wauguzi ili kuhakikisha wanatoa huduma bora kwa Wananchi na kuwapongeza wauguzi wote kwa kazi wanayoifanya ya kuwahudumia Wananchi.
Kwa upande wake Mganga Mkuu wa mkoa wa Kigoma Damas Kayela amesema wataendelea kushirikiana na wauguzi katika kutatua changamoto zinazowakabili ili kuimarisha huduma za afya kwa wananchi.
Naye mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM )Wilaya ya Buhigwe Eng Dyegula ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuboresha huduma za Afya kwa kuboresha miundominu na kuongeza vituo vya Afya kwa ajili ya kuwapatia wananchi huduma zilizo bora.
Adoneth Josephat na Hamis Bilanyobeye ni wakazi wa Wilaya ya Buhigwe kwa pamoja wameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikiongozwa na Dkt Samia Suluhu Hassani kwa kumaliza changamoto yao ya umbali wa kituo cha Afya na kuomba kutatuliwa changamoto ya upungufu wa Wauguzi katika vituo vyao vya Afya.
Mji Mpya wa Bwega-Ofisi za Mkurugenzi
Postal Address: P.O.Box 443 Buhigwe
Simu Ya Mezani: 0282988460
Simu ya mkononi: (+255) 782 500 333
Barua Pepe: ded@buhigwedc.go.tz