• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za ofisi |
Buhigwe District Council
Buhigwe District Council

Jamuhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Msingi Mkuu
    • Mpango Mkakati
  • Utawala
    • Muundo Wa Utawala
    • Idara
      • Utawala Na Utumishi
      • Mipango, Takwimu Na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha Na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Secondari
      • Maji
      • Mifugo Na Uvuvi
      • Ardhi Na Maliasili
      • Maendeleo Ya Jamii Na Ustawi Wa Jamii
      • Ujenzi Na Zimamoto
      • Kilimo,Umwagiliaji Na Ushirika
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi Wa Ndani
      • Habari Na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kiutalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
      • Kuonana na Mhe.Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Inayotarajiwa Kufanywa
    • Miradi Inayoendelea Kufanywa
    • New Planned Project
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Other Fomu
    • MpangoKazi
    • Baraza-Madiwani
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Lishe Bora kwa Maisha Yote

Posted on: March 2nd, 2020

Kama wadau wa lishe katika Wilaya yetu ya Buhigwe tunapaswa kuwajibika kila mmoja kwa eneo lake kuhakikisha udumavu kwa watoto unatoweka kwa kuhakikisha lishe bora inatolewa kwa kuzingatia makundi makuu matano ya vyakula yaani wanga, protini, vitamini, mafuta na madini ambavyo vinapatikana katika maeneo yetu kwa gharama ndogo. Hayo yalisemwa na Mhe. Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe Col. Michael M. Ngayalina wakati akifungua kikao cha kamati ya lishe kilichofanyika katika ukumbi wa ofis ya Mkurugenzi Mtendaji Buhigwe eneo la Bwega hivi karibuni. 

Kwa upande wake Afisa lishe wilaya; Madam Theodora Thomas alieleza makundi makuu matano ya vyakula ambayo yanapaswa kuzingatiwa katika lishe hasa kwa watoto.

  1. Nafaka, Mizizi na Ndizi
  • mchele, mahindi, mtama, ulezi, ngano, uwele, viazi vikuu, viazi vitamu, mihogo, magimbi, viazi mviringo, na Ndizi

Virutubishi: Wanga

  • Huupatia mwili nguvu za kuweza kufanya kazi

2.Vyakula vya aina ya mikunde na vyenye asili ya wanyama

  • Maharage, kunde, mbaazi, soya, karanga,njegere, njugu mawe,dengu, choroko, asili ya wanyama ni: nyama, mayai, samaki, dagaa, kumbikumbi, senene, maziwa na nzige.

Virutubishi: Protini

  • Hujenga mwili. Huwezesha mwili kutengeneza seli nyingine.


3.Mboga-mboga

  • mchicha, majani ya kunde, majani ya maboga, kisamvu, matembele, spinachi, mgagani, mlenda, mnavu, mchunga, karoti, pilipili hoho, nyanya chungu, biringanya, bamia, kabichi, figiri, sukuma wiki na chainizi.

  • Huupa mwili kinga imara dhidi ya maradhi mbalimbali.


4.Matunda

  • mapera, maembe, machungwa, papai, nanasi, zambarau, zabibu, mapesheni, machenza, ubuyu, ukwaju, limao, ndizi, matango, matikiti maji, parachichi n.k

  • Huupa mwili kinga dhidi ya maradhi.
  • Husaidia kwa baadhi ya virutubishi kutumika kwa ufasaha zaidi mwilini.


5.Mafuta na Sukari

  • mafuta ya kupikia, ufuta, karanga, mbegu za alizeti, siagi, samli, nyama yenye mafuta, sukari ni: asali, miwa, vyakula vinavyotengenezwa kwa sukari nyingi kama jamu, keki, n.k

virutubishi: mafuta

  • Huupa mwili nguvu.
  • Husaidia ufyonzwaji wa vitamini A,D,E na K.


    Maji???????

    Maji hayakuwekwa kwenye kundi lolote la chakula kwa sababu hayana virutubishi. Ni muhimu kunywa maji safi na salama kwani yanarahisisha umeng'enyaji wa chakula, kusafirisha virutubishi na kutoa uchafu ambao hutengenezwa mwilini wakati mwili unafanya kazi zake. Asilimia kubwa ya mwili ni maji hivyo ni vyema kunywa maji mara kwa mara ili kuwa na afya bora.


    Kumbuka:

    ni vema kula vyakula vyenye mchanganyiko wa kila kundi la chakula ili mwili uwe na afya nzuri, na kutopatwa na maradhi mara kwa mara, pia kunywa maji safi na salama wakati wote unapohitaji. Alisema Theodora.



Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI - 04.07.2023 June 23, 2023
  • KILA KHERI DARASA LA SABA September 12, 2023
  • TANGAZO LA AJIRA - OKTOBA 2023 October 09, 2023
  • TANZIA February 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • DED BUHIGWE ATEMBELEA VITUO VYA UANDIKISHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA.

    May 05, 2025
  • MATOKEO 2024 WALIMU NA WANAFUNZI WAPONGEZWA.

    April 17, 2025
  • BABA ASKOFU EMMANUEL BWATA AITIKIA WITO WA MKURUGENZI BUHIGWE.

    April 14, 2025
  • SHEREHE YA KUWAAGA WATUMISHI NA KUWAKARIBISHA WATUMISHI BUHIGWE YAFANA.

    April 13, 2025
  • Angalia zote

Video

Hospitali ya Wilaya ya Buhigwe kuanza kutoa huduma za Afya
Video Zaidi

Kurasa Za Karibu

  • Kuhamisha Mwanafunzi
  • Tovuti ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • FFARS USER GUIDE
  • PlanRep Documentation
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • Kata Zetu
  • Wahe. Madiwani
  • BEMIS

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Bunge La Tanzania
  • Ikulu
  • Bodi Ya Manunuzi na Ugavi
  • Wizara ya Ardhi
  • Wizara ya Elimu, Sayansi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Mji Mpya wa Bwega-Ofisi za Mkurugenzi

    Postal Address: P.O.Box 443 Buhigwe

    Simu Ya Mezani: 0282988460

    Simu ya mkononi: (+255) 782 500 333

    Barua Pepe: ded@buhigwedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma
    • Mwanzo

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Buhigwe. Haki zote zimehifadhiwa