• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za ofisi |
Buhigwe District Council
Buhigwe District Council

Jamuhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Msingi Mkuu
    • Mpango Mkakati
  • Utawala
    • Muundo Wa Utawala
    • Idara
      • Utawala Na Utumishi
      • Mipango, Takwimu Na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha Na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Secondari
      • Maji
      • Mifugo Na Uvuvi
      • Ardhi Na Maliasili
      • Maendeleo Ya Jamii Na Ustawi Wa Jamii
      • Ujenzi Na Zimamoto
      • Kilimo,Umwagiliaji Na Ushirika
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi Wa Ndani
      • Habari Na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kiutalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
      • Kuonana na Mhe.Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Inayotarajiwa Kufanywa
    • Miradi Inayoendelea Kufanywa
    • New Planned Project
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Other Fomu
    • MpangoKazi
    • Baraza-Madiwani
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Kikao cha Baraza la Biashara

Posted on: December 12th, 2017

Kikao kilifunguliwa mnamo saa 10:24 asubuhi na Mwenyekiti wa Baraza la Biashara la wilaya Col Marco E. Gaguti na kukaribisha wajumbe wa baraza ambao ni Sekta Binafsi na Sekta ya Umma pamoja na wageni kutoka mkoani ambao ni meneja wa mradi LIC, Afisa Biashara wa Mkoa na Mratibu wa Baraza la Biashara la Taifa (TNBC).

Kikao kiliendelea kwa kuendeshwa na Sekretarieti ya wilaya ambapo wajumbe walijitambulisha mmoja mmoja na kumalizia na meza kuu ambapo ilikuwa na Mwenyekiti wa Baraza (DC), Katibu (DED), Mwenyekiti wa Halmashauri na Mwenyekiti wa TCIAA wilaya ya Buhigwe.

Kutoka kushoto mwa picha ni Mwenyekiti wa TCIAA wilaya ya Buhigwe(Ndg. Azalia A. Kolobo), Elihuruma J. Nyella (Katibu wa kikao) akifatiwa na Mhe. Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe (Col Marco E. Gaguti) ambaye ni Mwenyekiti wa Baraza la biashara wilaya ya Buhigwe, na mwisho ni Mwenyekiti wa Halmashauri (Mhe. Venance Kigwinya).

Sekretarieti iliendelea kwa kusoma na kuhakikisha Agenda zilizotakiwa kujadiliwa siku hiyo, wajumbe walizipitia na kuhakiki kisha Sekretarieti ilisoma muhtasari wa kikao kilichopita cha Baraza la Biashara cha tarehe 29/9/2017. Baada ya Sekretarieti kuongoza wajumbe wa Baraza katika kusoma muhtasari huo ndipo kipengere cha yatokanayo kilifuata huku Mwenyekiti akifuatilia kwa ukaribu maazimio na utekelezaji wake.

AGENDA:

 Urasimishaji wa Biashara wilaya ya Buhigwe.

Agenda hii iliwasilishwa na Afisa Biashara wa Mkoa ambapo alielezea umuhimu wa urasimishaji wa biashara unafanya wafanyabiashara kuwa rasmi na kutambulika nchini katika biashara zao. Aliendelea kwa kuwasisitiza wafanyabiashara kujipatia TIN namba kwa kuwa ni bure kwa watu wote ili kurahisisha urasimishwaji huo wa Biashara. Wajumbe wa Sekta binafsi waliulizwa maswali kama tofauti kati ya TIN namba na kujisajili na majibu yote yalijibiwa na Afisa Biashara wa Mkoa.

Agenda hii ilifungwa na Mwenyekiti kwa kutoa azimio kwamba LIC na wadau wengine wasaidie ili elimu hii iwafikie wafanyabiashara wote.

Afisa Biashara wa Mkoa akieleza umuhimu wa urasimishaji wa biashara.

Mpango mkakati wa kufanya mnada wa Wilaya ya Buhigwe kuendelea kufanya kazi. Katika agenda hii Afisa mifugo alielezea kwa kina kwa wajumbe na kuelezea kuwa jitihada za kuzuia mifugo isivushwe nje ya nchi ni kubwa sana ingawa inakwamishwa kutokana na maafisa mifugo kuwa wachache wilaya nzima ya Buhigwe.

Zoezi la upigaji chapa wa mifugo.

Afisa mifugo alifafanua kuhusu zoezi hili kwa wajumbe na kuelezea umuhimu wa kufanya au kupiga chapa. Alitoa wito kwa wafugaji na wafanyabisahara wa mifugo kupeleka ng’ombe kwenye chapa kwa ajili ya usalama, utambulizi na uhalali wa mifugo hiyo. Agenda hii ilifungwa na Mwenyekiti kwa kutoa maazimio kwamba mnada uanze ifikapo tarehe 03.01.2018, kufanya doria ili kudhibiti mifugo kutoroshwa nchi za jirani, wafanyabiashara waainishiwe njia maalumu watakazozitumia kupitisha mifugo yao.

Afisa mifugo(W) Ndg. Kenneth Tefurukwa akieleza umuhimu wa zoezi la upigaji chapa mifugo.

Mpango mkakati wa kuboresha mnyororo wa thamani.

Afisa kilimo alifafanua zao la mchikichi na ndipo wajumbe wakaanza kuchangia mada na wakahoji kwamba kwa nini zao la kahawa halikuainishwa na kupewa kipaumbele. Ndipo mwenyekiti aliamuru kwamba mkakati kuhusu vipaumbele vya wilaya ya Buhigwe viainishwe.

Upatikanaji wa pembejeo za ruzuku.

Katika agenda hii ilionekana wakulima wanafata mbolea kwa wakala mkubwa wilaya ya Kasulu hivyo wajumbe wakaomba apatikane wakala katika wilaya yetu ya Buhigwe ili kuondoa usumbufu kwa wakulima. Agenda hii ilifungwa na mwenyekiti kwa kutoa azimio kwamba wananchi (wakulima) wajiorodheshe na kwenda kununua mbolea kwa wingi, na pia alitoa fursa kwa wafanyabiashara watakaoweza kuwa mawakala ili kutatua tatizo hili.

Ushirikishwaji wa sekta binafsi katika maamuzi yanayofikiwa na sekta ya umma. 

Wajumbe wa sekta binafsi walihoji kwamba ushirikishwaji haupo kwasababu ya kuona matangazo kuhusu ununuzi wa viwanja na hawajawahi kushirikishwa. Katibu wa kikao alikiri kutokea kwa jambo hilo na kuwatoa hofu wajumbe kwamba mikataba iko tayari na zoezi hilo litaanza hivi karibuni. Mwenyekiti alifunga agenda hii kwa kusema kwamba mawasiliano baina ya sekta hizi mbili yaboreshwe.

Kikosi kazi kiwezeshwe ili kimalizie zoezi la ufatiliaji wa maazimio yanayofikiwa na vikao vya Baraza la Biashara.

Wajumbe walihoji kwamba kazi za ufatiliaji wa maazimio zimeshindwa kufanyika kwasababu kulikuwa hakuna uwezeshwaji kwa kikosi kazi hivyo iliamuliwa kikosi kazi hiki kisitolewe bali kimalizie kazi ili kilete mrejesho baraza la Biashara lijalo. Pia manager (LIC) aliahidi hadi tarehe 20/12/2017 itakuwa imewezesha kikosi kazi hiki.

Uanzishwaji, uendelezwaji na usajili wa viwanda vidogo na vya kati.

Agenda hii iliibuliwa kwa kuwa na umuhimu wa Tanzania ya Viwanda. Ni agizo la kitaifa kwamba kila mkoa uwe na viwanda visivyopungua 100. Mwenyekiti alishauri ili agizo hili liweze kutimia yapatikane maeneo yaliyopimwa ili iwe rahisi hata wawekezaji wakija iweze kuwa rahisi kwao.

Changamoto zinazokwamisha masoko ya mpakani kufanya kazi.

Agenda hii iliibua majadiliano ambapo ilionekana masoko ya mpakani yana changamoto za wanajeshi kuchukua ushuru kwa wafanyabiashara. Swala hili limekuwa kikwazo sana na kufanya baadhi ya wafanyabiashara hata wa nchi jirani kuogopa kufika kwenye masoko yetu hayo. Mwenyekiti alifunga agenda hii kwa kuwatoa hofu wajumbe na kwamba swala hili litafanyiwa kazi hivyo wafanyabiashara wafanye biashara kwa amani.

Baada ya agenda hizi kujadiliwa kulikuwa na taarifa kutoka Sekretarieti kuhusu ushuru wa huduma. Wafanyabiashara walielezwa kwamba wajiandae kwa maana elimu hii itawafikia. Ushuru wa huduma ni muhimu kwasababu huongeza mapato kwenye halmashauri na kwamba ipo kwa mujibu wa sheria ya serikali za mitaa. Hivyo wafanyabiashara walisisitizwa kujiandaa na elimu hiyo itakayotolewa.

Baada ya taaifa hiyo kulikuwa na agenda za ziada ambazo zilielezewa na wageni kutoka mkoani kama Afisa biashara wa mkoa na afisa sera (LIC).

  • Kuendelea kwa mabaraza ya Biashara baada ya LIC kuondoka.
  • Hoja hii ilionekana muhimu kwasababu mradi huu utaondoka hivyo mabaraza yanatakiwa kusimama yenyewe bila msaada wa mradi huu. Ilishauriwa kwamba bajeti ya baraza iwekwe kwenye bajeti ya halmashauri ili kuwezesha vikao vya baraza kukaa na kujadili maslahi ya sekta binafsi na umma na wilaya kwa ujumla. Afisa Biashara Mkoa alisisitiza pia mratibu wa Baraza awe Afisa Biashara wa wilaya ili kuendeleza shughuli zote zitakazohusiana na mabaraza haya hata mradi wa LIC wakiondoka

MENGINEYO:

  • Jengo la One Stop Business Centre (OSBC) ikiwa na ofisi ya Afisa Biashara, TCCIA, TRA waweze kufanya kazi kwa pamoja. Pia watakao hudumu wafanyiwe mafunzo ili kuleta ufanisi kwenye kazi katika kituo hicho.
  • Maboresho katika utozaji wa ushuru wa magari hususani Munanila.

Mwenyekiti wa Baraza la Biashara alimalizia kikao kwa kukaribisha wageni wa mkoani washukuru kwa dakika 2 kila mtu.

  • Mjumbe (TNBC) alisisitiza kwamba wajumbe wawe na barua na pia wawe wajumbe wa kujituma kwa kuwahi kwenye vikao na kuchangia hoja zinazojadiliwa kwa maslahi ya wafanyabiashara wanao wawakilisha.
  • Manager (LIC) aliongelea kwamba wakiwa wanajiandaa kuondoka kwenye mradi wanataka kuacha alama (kumbukumbu) Buhigwe.
  • Afisa Biashara mkoa nae alimshukuru Mwenyekiti kwa nafasi aliyopewa na kumsifia kwamba alimaliza kikao kwa muda huku agenda zote zikiwa zimejadiliwa.
  • Alisisitiza swala la urasimishaji wa biashara kwamba wafanayabiashara wajiandae na zoezi hili.
  • One Stop Business Centre (OSBC) ijengwe na itumike kabla mradi wa LIC haujaondoka.
  • Na mwisho sekretarieti ijitahidi katika kuandaa taarifa mbalimbali ikiwemo za kikosi kazi na mihtasari mapema ili kuondoa mkanganyiko wa taarifa.
  • Mwenyekiti wa TCCIA wilaya alishukuru wajumbe kwa kuhudhuria kikao na pia aliomba uongozi mpya wa wajumbe ambao utalenga wafanyabiashara kanda zote za wilaya ya Buhigwe wateuliwe ili kufanya Baraza liwe na mashiko na uwakilishi mpana kuliko ulivyo sasa hivi.
  • Mwisho kabisa katibu (DED) nae alishukuru wajumbe na Mwenyekiti kwa kuendesha kikao vizuri na kuomba agenda zilizojadiliwa zifanyiwe kazi ili litakapokuja Baraza lingine ziwasilishwe.

Mwenyekiti wa halimashauri alimalizia kwa kushukuru wajumbe wa Baraza na waalikwa na ndipo Mwenyekiti alifunga kikao cha Baraza la Biashara mnamo saa 16:45 jioni hadi kikao kingine mwezi wa 3.

MAAZIMIO:

Na.
Ajenda
Maazimio
1.
Urasimishaji wa biashara Wilaya ya Buhigwe.
  • Iliazimiwa kuwa elimu itolewe kwa wafanyabiashara kuhusiana na zoezi la urasimishaji wa biashara.
2.
Mpango mkakati wa kuufanya mnada wilaya ya Buhigwe kuendelea kufanya kazi.
  • Kikao kiliazimia kuwa kufikia tarehe 19.12.2017 taarifa zitolewe kupitia matangazo kuhusiana na kuanza kutumika kwa mnada wa Wilaya ya Buhigwe.
  • Njia maalumu za kupitisha mifugo ziainishwe.
  • Doria zifanyike kuthibiti mifugo kutoroshwa nchi jirani.
  • Pia iliazimiwa kuwa kufikia tarehe 03.01.2018 munada uanze kufanya kazi.
3.
Mpango mkakati wa kuboresha mnyororo wa thamani.
  • Kikao kilitoa maelekezo kwa wataalamu wakae pamoja na wadau wa kilimo ili kubainisha ni mazao yapi yapitishwe katika mnyororo wa thamani na yawe ni mazao yanayositawishwa Wilaya nzima.
4.
Ushirikishwaji wa sekta binafsi katika maamuzi yanayofikiwa na sekta ya umma.
  • Kikaon kiliazimia kuwa mawasiliano baina ya sekta ya umma na binafsi yaboreshwe kwa kutoa taarifa ya maamuzi yanayofikiwa.
  • Kikao kiliazimia kuwa ndani ya wiki mbili yaani kufikia tarehe 26.12.2017 wataalamu toka halmashauri wakae na wananchi ili kutoa taarifa na taratibu kamili za uuzwaji wa vibanda vya biashara eneo la Munanila.
5.
Kikosi kazi kiwezeshwe ili kimalizie zoezi la ufuatiliaji wa maazimio yanayofikiwa katika vikao vya baraza la biashara.
  • Kikao kiliazimia kuwa ufuatiliaji wa ufadhili uratibiwe kwa kufikisha andiko ofisi za LIC Kigoma ili kufikia tarehe 20.12.2017 majibu yaweze tolewa na uongozi wa LIC.
6.
Upatikanaji wa pembejeo za ruzuku.
  • Kikao kiliazimia kuwa wataalamu wawaelimishe wakulima na wananchi kwa ujumla gharana na taratibu za kupata pembejeo hizo.
  • Pia kutokuwepo kwa mawakala wa pembejeo za kilimo ilichukuliwa kama fursa ya uwekezaji katika sekta ya kilimo na kuwaasa wafanyabiashara kuchangamkia fursa hiyo ili kutatua changamoto zinazo wakabili wakulima.
7.
Uanzishwaji, uendelezwaji na usajili wa viwanda vidogo na kati.
  • Iliazimiwa kuwa tarehe 10.01.2018 kiandaliwe kikao maalumu cha wadau kujadili mikakati ya uanzishwaji wa viwanda Wilaya ya Buhigwe.
  • Pia katika kikao hicho iundwe timu maalumu ambayo itaratibu na kuainisha mikakati ya kuanzisha viwanda Wilaya ya Buhigwe.
8.
Zoezi la upigaji chapa kwenye mifugo.
  • Kikao kiliazimia kuwa wataalamu watoe elimu juu ya zoezi la utambulisho wa mifugo kwa kuwekewa chapa kulingana na maelekezo ya Wizara.
9.
Changamoto zinazokwamisha masoko ya mpakani kufanya kazi.
  • Kikao kiliazimia kuwa changamoto ama vikwazo vinavyokwamisha shughuli za masoko ya mpakani kufanya kazi ziainishwe.
  • Changamoto za mda mfupi Mwenyekiti kwa kushilikiana na wadau alihaidi kuzishughurikia.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI - 04.07.2023 June 23, 2023
  • KILA KHERI DARASA LA SABA September 12, 2023
  • TANGAZO LA AJIRA - OKTOBA 2023 October 09, 2023
  • TANZIA February 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • DED BUHIGWE ATEMBELEA VITUO VYA UANDIKISHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA.

    May 05, 2025
  • MATOKEO 2024 WALIMU NA WANAFUNZI WAPONGEZWA.

    April 17, 2025
  • BABA ASKOFU EMMANUEL BWATA AITIKIA WITO WA MKURUGENZI BUHIGWE.

    April 14, 2025
  • SHEREHE YA KUWAAGA WATUMISHI NA KUWAKARIBISHA WATUMISHI BUHIGWE YAFANA.

    April 13, 2025
  • Angalia zote

Video

Hospitali ya Wilaya ya Buhigwe kuanza kutoa huduma za Afya
Video Zaidi

Kurasa Za Karibu

  • Kuhamisha Mwanafunzi
  • Tovuti ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • FFARS USER GUIDE
  • PlanRep Documentation
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • Kata Zetu
  • Wahe. Madiwani
  • BEMIS

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Bunge La Tanzania
  • Ikulu
  • Bodi Ya Manunuzi na Ugavi
  • Wizara ya Ardhi
  • Wizara ya Elimu, Sayansi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Mji Mpya wa Bwega-Ofisi za Mkurugenzi

    Postal Address: P.O.Box 443 Buhigwe

    Simu Ya Mezani: 0282988460

    Simu ya mkononi: (+255) 782 500 333

    Barua Pepe: ded@buhigwedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma
    • Mwanzo

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Buhigwe. Haki zote zimehifadhiwa