• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za ofisi |
Buhigwe District Council
Buhigwe District Council

Jamuhuri Ya Muungano Wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Msingi Mkuu
    • Mpango Mkakati
  • Utawala
    • Muundo Wa Utawala
    • Idara
      • Utawala Na Utumishi
      • Mipango, Takwimu Na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha Na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Secondari
      • Maji
      • Mifugo Na Uvuvi
      • Ardhi Na Maliasili
      • Maendeleo Ya Jamii Na Ustawi Wa Jamii
      • Ujenzi Na Zimamoto
      • Kilimo,Umwagiliaji Na Ushirika
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi Wa Ndani
      • Habari Na Mawasiliano
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kiutalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Wah. Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
      • Kuonana na Mhe.Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Inayotarajiwa Kufanywa
    • Miradi Inayoendelea Kufanywa
    • New Planned Project
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Other Fomu
    • MpangoKazi
    • Baraza-Madiwani
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

DC NGAYALINA AONGOZA KIKAO CHA TATHIMINI YA VIASHIRIA VYA MKATABA WA LISHE WILAYANI BUHIGWE

Posted on: May 31st, 2024




Kikao hicho kimefanyika Mei 31,2024 katika ukumbi wa utawala Hospital ya Wilaya ya Buhigwe kikiwa na lengo la kwenda kuhamasisha wazazi na walezi kuchangia vyakula mashuleni.

 Walioshiriki kikao hicho ni Weo's Dhro Elimu Msingi na Sekondari kwakuwa wao wanahisika kwa ujumla wao kutoa Elimu na uhamasishaji katika jamii au wazazi na walezi wa watoto ili wajue umhimu wa wanafunzi kupata chakula mashuleni.


"Ndugu washiriki; Sote tunapaswa kufahamu lishe ni suala mtambuka na utapiamlo katika jamii ni matokeo ya mkusanyiko wa matatizo mengi. Matatizo hayo yanaweza kusababishwa na ulaji duni na mtindo wa maisha usiofaa, maradhi mbalimbali, kutokuwa na uhakika wa chakula, matunzo duni ya akina mama wajawazito na watoto, mazingira machafu, rasilimali haba na mgawanyo usiokuwa na uwiano sahihi kijinsia, umaskini wa kipato, machafuko ya kisiasa na hata sera zisizotambua umuhimu wa lishe kwa maendeleo ya mwanadamu na taifa kwa ujumla wake.



Kila familia inapaswa kufahamu umuhimu wa lishe bora. Hii ni kwasababu takriban nusu ya vifo vya watoto chini ya miaka mitano kila mwaka hutokana na ukosefu wa lishe bora, unaosababisha kudhoofika kwa kinga mwili hivyo kupelekea mwili kushindwa kupambana na magonjwa. Vilevile lishe duni huwaweka wanawake wajawazito katika mazingira hatarishi yanayoweza kusababisha kujifungua watoto njiti, Watoto wafu, watoto wenye mtindio wa ubongo au hata kuharibika kwa mimba na vifo vya akina mama wakati au baada ya kujifungua.


Wataalam wanatuambia kuwa watoto waliopata huduma bora na sahihi za lishe, katika kipindi cha siku 1,000 za mwanzo wa uhai wao (kwa maana ya miezi tisa ya mimba na mpaka kufikia umri wa miaka miwili baada ya kuzaliwa) wanapata faida zitakazodumu katika maisha yao yote ikiwa ni pamoja na maendeleo mazuri ya ukuaji wa ubongo, uwezo mzuri wa kukabiliana na maradhi, uwezo mkubwa wa akili za utambuzi (higher IQ), uwezo mkubwa na ufanisi.


Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI - 04.07.2023 June 23, 2023
  • KILA KHERI DARASA LA SABA September 12, 2023
  • TANGAZO LA AJIRA - OKTOBA 2023 October 09, 2023
  • TANZIA February 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • DED BUHIGWE ATEMBELEA VITUO VYA UANDIKISHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA.

    May 05, 2025
  • MATOKEO 2024 WALIMU NA WANAFUNZI WAPONGEZWA.

    April 17, 2025
  • BABA ASKOFU EMMANUEL BWATA AITIKIA WITO WA MKURUGENZI BUHIGWE.

    April 14, 2025
  • SHEREHE YA KUWAAGA WATUMISHI NA KUWAKARIBISHA WATUMISHI BUHIGWE YAFANA.

    April 13, 2025
  • Angalia zote

Video

Hospitali ya Wilaya ya Buhigwe kuanza kutoa huduma za Afya
Video Zaidi

Kurasa Za Karibu

  • Kuhamisha Mwanafunzi
  • Tovuti ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • FFARS USER GUIDE
  • PlanRep Documentation
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • Kata Zetu
  • Wahe. Madiwani
  • BEMIS

Tovuti Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Bunge La Tanzania
  • Ikulu
  • Bodi Ya Manunuzi na Ugavi
  • Wizara ya Ardhi
  • Wizara ya Elimu, Sayansi

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Mji Mpya wa Bwega-Ofisi za Mkurugenzi

    Postal Address: P.O.Box 443 Buhigwe

    Simu Ya Mezani: 0282988460

    Simu ya mkononi: (+255) 782 500 333

    Barua Pepe: ded@buhigwedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Waliotembelea

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma
    • Mwanzo

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya Buhigwe. Haki zote zimehifadhiwa